WAOMBAJI KAZI WAMETAKIWA KUJIANDAA WANAPOENDA KWENYE USAILI

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira, Bw. Xavier Daudi (kushoto) akifafanua jambo kwa Waandishi wa habari (hawapo pichani) na kulia ni Mwenyekiti wa Sekretarieti ya Ajira, Bw. Bakari Mahiza.

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Bw. Xavier Daudi amesema ofisi yake hivi sasa itakuwa ikitoa ratiba ya usaili mapema kila mara ili kuwawezesha wasailiwa kuwa na muda wa kutosha kujiandaa kabla ya kwenda kwenye usaili husika.
Amesema hayo leo wakati akiongea na mwandishi wa habari ofisini kwake alipokuwa  akitoa ratiba ya usaili kwa mwezi Septemba, 2012 pamoja na tangazo la kuita kazini waombaji waliofaulu usaili uliopita. Aliongeza kuwa ili msailiwa aweze kufanya vizuri katika usaili pamoja na vigezo vya kitaaluma alivyonavyo bado anatakiwa kujiandaa vyema na kujiamini anapojibu maswali wakati anapokuwa kwenye usaili.
Daudi amesema hivi sasa dunia imekuwa ya utandawazi na fursa za ajira ni za ushindani zaidi, maana wahitimu hivi sasa ni wengi na hawana ajira hivyo ni vyema kwa wahitimu wanapoomba nafasi za kazi na kuitwa kwenye usaili wawe wamejiandaa vya kutosha ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kupata ajira.
Katibu amesema usaili kwa mwezi Septemba,  utaanza tarehe 18 Septemba  hadi 5 Oktoba, 2012 kwa taasisi zifuatazo; Wakala wa Barabara (TANROADS), Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), TEMESA, ADEM, CARMATECH, NEEC (UWEZESHAJI), Chuo cha Utalii, Chuo cha Diplomasia, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Wizara ya Fedha (PFMRP) EPZA, na Maafisa Tarafa.
Amesema kwa maelezo zaidi ya nafasi hizo na wapi usaili utafanyika ni vyema waombaji wakaperuzi tovuti ya Sekretarieti ya Ajira pamoja na tovuti za Taasisi husika na kufungua tangazo la kuitwa kwenye usaili  ili kuiona ratiba nzima ya tarehe ya mchujo na usaili kama zinavyoonekana katika tangazo lenye orodha ya majina ya kuitwa kwenye usaili.
Aidha, amesisitiza ni muhimu kwa waombaji kuzingatia masharti ya tangazo pindi wanapoenda kwenye usaili kwani ni njia mojawapo ya kujua msailiwa amejiandaa kwa kiasi gani.
Wakati huohuo, Katibu amewataka waombaji wa nafasi za kazi waliofanya usaili kuanzia tarehe 7 hadi 31, Agosti, 2012 katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Chuo cha Biashara  (CBE), Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, Chuo cha Maji (WDMI), Chuo cha Mipango Dodoma (IRDP), Chuo cha Serikali za Mitaa- Hombolo, COASCO, Tume ya Vyuo Vikuu (TCU), Tume ya Mionzi (TAEC), Taasisi ya Utafiti wa Samaki (TAFIRI), Wakala wa Mbegu (TOSCI), Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TASUBA)  kuangalia majina yao katika tovuti ya Sekretarieti ya Ajira pamoja na taasisi husika ili kujua waliofaulu.
Amesema kwa waliofaulu usaili wanatakiwa kuripoti kwa Mwajiri katika muda ambao umeainishwa kwenye barua zao za kupangiwa vituo vya kazi wakiwa na vyeti halisi (Originals) vya masomo kuanzia kidato cha nne na kuendelea ili vihakikiwe na mwajiri kabla ya kupewa barua ya ajira. Aidha, barua za kuwapangia vituo vya kazi zimetumwa kupitia anuani zao za posta.
Alimalizia kwa kusema kuwa, kwa wale ambao hawataona majina yao  katika tangazo husika  watambue kuwa maombi yao hayakufanikiwa na wasisite kuendelea kuomba mara nafasi za kazi zitakapotangazwa tena.

Views: 832

Tags: ajira

Comment

You need to be a member of Global Publishers to add comments!

Join Global Publishers

Comment by David Wagwene on September 17, 2012 at 11:01pm

Taarifa nzuri lakini maana unaweza kuwa na CV nzuri ukakuta bado unakosa kazi kumbe kwa sababu ya makosa madogomadogo

Comment by julius manning on September 15, 2012 at 9:36am

nimekubali

Comment by steven emmanuel on September 15, 2012 at 8:50am

hii nzuri maana watu weng wanaenda kwnye usaili bila maandaliz yoyote mwisho wa siku hakikosa lawama bora wametoa taarifa mapema

ADVERTISEMENT


Advertisement

 

Forum

KIPIGO CHA BAO 2-1 KWA MAN UTD, KOSA LA MWAMUZI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Mohammed Mar 26. 6 Replies

JE, NI KWELI KWAMBA KIPIGO CHA BAO 2-1 ILICHOKIPATA MAN UTD KUTOKA KWA REAL MADRID USIKU WA KUAMKIA LEO LAWAMA ZOTE ZIMWENDEE MWAMUZI WA MCHEZO AU MAN UTD WAJILAUMU WENYEWE? TUPE MAONI YAKO!!!

HALI INAYOENDELEA BUNGENI, SPIKA NA NAIBU WAKE WAMESHINDWA KUONGOZA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Ali Abdalla Ali Apr 22. 20 Replies

Tumeshuhudia kwa siku za hivi karibuni hali halisi iliyokuwa inatokea katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, kwa hali hii ni ishara kuwa Spika na Naibu wake washindwa kuliongoza bunge hilo?

VURUGU ZA CCM NA CHADEMA KUGOMBEA MLINGOTI WA BENDERA DODOMA, NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Phinehas Rishiansia Kileo May 3. 6 Replies

Wafuasi wa CCM wakimshambulia mfuasi wa Chadema mkoani Dodoma…

Tags: BENDERA, WA, DODOMA, NANI, KULAUMIWA?

VURUGU ZINAZOENDELEA HAPA NCHINI NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by NELSON UVAMBE yesterday. 27 Replies

HIVI KARIBUNI KUMEKUWEPO UPOTEVU WA AMANI HAPA NCHINI PAMOJA NA WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI. MKOANI KAGERA WANANCHI WENYE HASIRA WALIWAUA POLISI, IJUMAA ILIYOPITA WAKULIMA NA WAFUGAJI HUKO WILAYANI KILOSA WALIZUA VURUGU NA KUFUNGA BARABARA,…

MRISHO NGASSA KUPELEKWA SIMBA SC BILA RIDHAA YAKE, JE NI HALALI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Domino Bagambisa Jan 21. 17 Replies

Kiungo hatari wa Azam FC, Mrisho Ngassa leo amepelekwa Simba SC kwa mkopo na timu yake…

Tags: SOKA

hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Started by Gysper in Siasa. Last reply by Jamal amor May 9. 24 Replies

 hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Kauli Ya JK kuwa Mauaji ya Arusha ni "Bahati Mbaya"

Started by Kulikoni Ughaibuni in Siasa. Last reply by richardngeze Feb 12. 12 Replies

Tanzania tuna tatizo kubwa.Hakuna haja ya kunyoosheana vidole as to nani amechangia tatizo hilo bali cha muhimu na haraka ni namna tutakavyoweza kutatua tatizo hili.Nisimung'unye maneno: tatizo kubwa linaloikabili ni kuwa na Rais ambaye takriban…

Latest Activity

tina babi left a comment for ahmedinhoalimchox
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
36 seconds ago
tina babi left a comment for amani timoth mghase
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
41 seconds ago
tina babi left a comment for Micky Godwin Chetty
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
1 minute ago
tina babi left a comment for john mensah
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
1 minute ago
tina babi left a comment for saimon emmanuel lugenzi
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
1 minute ago
tina babi left a comment for peter lelo
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
2 minutes ago
tina babi left a comment for abubakar abdulkadir
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
2 minutes ago
tina babi left a comment for daniel samwel
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
3 minutes ago
tina babi left a comment for Jastin Mchena
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
3 minutes ago
tina babi left a comment for mohamedi saidi kinanda
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
3 minutes ago
tina babi left a comment for gabriel mbega
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
3 minutes ago
tina babi left a comment for Moud wa ukweli
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
3 minutes ago

© 2013   Created by Global Publishers.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service