VIJANA NCHINI WATAKIWA KUJIFUNZA ELIMU YA UJASIRIAMALI ILI KUONGEZA THAMANI KATIKA KAZI NA BIASHARA

Mwezeshaji katika mafunzo ya Ujasiriamali katika Wiki ya Ujasiriamali Duniani Austin Makani (kushoto) akitambulisha meza kuu wakati wa Hafla ya kukabidhi vyeti kwa wahitimu na kufunga Mafunzo hayo. Mgeni rasmi Mkuu wa Shule Kuu ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt. Ulingeta Mbamba (katikati), Mratibu Mipango wa Kitengo cha Ujasiriamali cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDEC) Bw. Elia Yobu (kulia), Makamu Mwenyekiti wa ZAYEE Bw. Omar Said Shabaan (wa pili kulia), Mkurugenzi Mkuu wa Professional Approach Development Bi. Lillian Secelela Madeje (kushoto) na Katibu Mkuu wa Shirika Lisilo la Kiserikali la ZAYEE (Zanzibar Association for Youth Education and Empowerment) Fatma Mabrouk Khamis (wa pili kushoto).

Pichani Juu na Chini ni Mkuu wa Shule Kuu ya Biashara ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt. Ulingeta Mbamba akitoa hotuba wakati wa kufunga mafunzo ya Ujasiriamali kwa Vijana yaliyoandaliwa na Asasi ya ZAYEE (Zanzibar Association for Youth Education and Empowerment) na kutolewa na Kitengo cha Ujasiriamali cha Chuo Kikuu cha DSM (UDEC).

Dkt. Mbamba amesema mafunzo hayo ni muhimu sana kwa vijana kwa kuwa yatawawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi, umahiri, tija zaidi na yatawasaidia sana katika kufanya shughuli zao za kila siku ziwe za kujiajiri wenyewe au kuajiriwa.

Katika mafunzo hayo jumla ya vijana 103 (68 kutoka Dar es Salaam na 35 kutoka Zanzibar) wamejifunza mambo mengi pamoja na Ujasiriamali, Fursa za Biashara zilizopo na Changamoto zake, Jinsi ya kupata Wazo la Biashara pamoja na Mpango wa Biashara.

Katibu Mkuu wa ZAYEE Bi. Fatma Mabrouk Khamis akiwapa nasaha wakufunzi wa mafunzo ya Ujasiriamali na kuwataka elimu waliyoipata hapo ikazae matunda katika kazi na biashara wanazozifanya ili kuongeza tija itakayosaidia kukuza uchumi binafsi wa Taifa. Pia ameahidi kuwafikia vijana wa Mikoani kuwapa mafunzo ya Ujasiriamali yatakayowezesha kuimarisha biashara zao.

Mwenyekiti wa Shirika Lisilo la Kiserikali la ZAYEE (Zanzibar Association for Youth Education and Empowerment) Bw. Masoud Salim Mohamed akizungumza na wahitimu hao ambapo ametoa fursa kadhaa na kuwataka kujijengea utamaduni wa kujiendeleza.

Mkurugenzi Mkuu wa Professional Approach Development Bi. Lillian Secelela Madeje akizungumzia umuhimu wa wajasiriamali kutumia michanganuo ya biashara katika kukuza biashara zao.

Katibu Mkuu wa ZAYEE Bi. Fatma Mabrouk Khamis akipokea cheti kufuzu mafunzo ya ujasiriamali wakati wa wiki ya Ujasiriamali Duniani kutoka kwa Dkt. Mbamba ambayo kwa Tanzania ndio mara ya kwanza kufanyika.

Pichani Juu na Chini ni baadhi ya washiriki wa mafunzo ya Ujasiriamali wakipokea vyeti baada ya kuhitimu.

Pichani Juu na Chini baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo yaliyomalizika jana jijini Dar es Salaam.

Meneja Maendeleo ya Biashara wa Kibo Palace Hotel Charity Githinji (kulia) akibadilishana mawazo na baadhi ya wahitimu wa mafunzo ya Ujasiriamali jinsi ya kupata wazo la biashara.

Wahitimu wa Global Entreprenuership Week Tanzania katika picha kumbukumbu pamoja na mgeni rasmi pamoja na wawezeshaji.

Bi. Fatma Mabrouk Khamis (wa pili kushoto) na Mwakilishi kutoka ILO pamoja na baadhi ya wahitimu.

Views: 93

Tags: BIASHARA, ELIMU, ILI, KATIKA, KAZI, KUJIFUNZA, KUONGEZA, NA, NCHINI, THAMANI, More…UJASIRIAMALI, VIJANA, WATAKIWA, YA

Comment

You need to be a member of Global Publishers to add comments!

Join Global Publishers

ADVERTISEMENT


Advertisement

 

Forum

KIPIGO CHA BAO 2-1 KWA MAN UTD, KOSA LA MWAMUZI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Mohammed Mar 26. 6 Replies

JE, NI KWELI KWAMBA KIPIGO CHA BAO 2-1 ILICHOKIPATA MAN UTD KUTOKA KWA REAL MADRID USIKU WA KUAMKIA LEO LAWAMA ZOTE ZIMWENDEE MWAMUZI WA MCHEZO AU MAN UTD WAJILAUMU WENYEWE? TUPE MAONI YAKO!!!

HALI INAYOENDELEA BUNGENI, SPIKA NA NAIBU WAKE WAMESHINDWA KUONGOZA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Ali Abdalla Ali Apr 22. 20 Replies

Tumeshuhudia kwa siku za hivi karibuni hali halisi iliyokuwa inatokea katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, kwa hali hii ni ishara kuwa Spika na Naibu wake washindwa kuliongoza bunge hilo?

VURUGU ZA CCM NA CHADEMA KUGOMBEA MLINGOTI WA BENDERA DODOMA, NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Phinehas Rishiansia Kileo May 3. 6 Replies

Wafuasi wa CCM wakimshambulia mfuasi wa Chadema mkoani Dodoma…

Tags: BENDERA, WA, DODOMA, NANI, KULAUMIWA?

VURUGU ZINAZOENDELEA HAPA NCHINI NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by NELSON UVAMBE on Monday. 27 Replies

HIVI KARIBUNI KUMEKUWEPO UPOTEVU WA AMANI HAPA NCHINI PAMOJA NA WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI. MKOANI KAGERA WANANCHI WENYE HASIRA WALIWAUA POLISI, IJUMAA ILIYOPITA WAKULIMA NA WAFUGAJI HUKO WILAYANI KILOSA WALIZUA VURUGU NA KUFUNGA BARABARA,…

MRISHO NGASSA KUPELEKWA SIMBA SC BILA RIDHAA YAKE, JE NI HALALI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Domino Bagambisa Jan 21. 17 Replies

Kiungo hatari wa Azam FC, Mrisho Ngassa leo amepelekwa Simba SC kwa mkopo na timu yake…

Tags: SOKA

hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Started by Gysper in Siasa. Last reply by Jamal amor May 9. 24 Replies

 hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Kauli Ya JK kuwa Mauaji ya Arusha ni "Bahati Mbaya"

Started by Kulikoni Ughaibuni in Siasa. Last reply by richardngeze Feb 12. 12 Replies

Tanzania tuna tatizo kubwa.Hakuna haja ya kunyoosheana vidole as to nani amechangia tatizo hilo bali cha muhimu na haraka ni namna tutakavyoweza kutatua tatizo hili.Nisimung'unye maneno: tatizo kubwa linaloikabili ni kuwa na Rais ambaye takriban…

© 2013   Created by Global Publishers.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service