“TUNAKUBALIANA na yote yaliyoandikwa humo na tuko tayari kumtunza na kumlea mtoto tutakayemchukua hapa kwa nguvu na juhudi zetu zote tukihakikisha anapata maisha yanayostahili.”
“Basi ni wakati wa ninyi kula kiapo mbele ya mwanasheria wetu.”
“Sawa sista,” walijibu kwa pamoja wakala kiapo na zoezi hilo lilipokamilika sista mkuu akauliza swali akiwataka wataje walihitaji mtoto wa jinsi gani na umri wake.
“Kuanzia miezi mitatu na awe wa jinsi ya kike.”
Hakujibu tena kitu akawataka wamfuate naye akaongoza moja kwa moja mpaka kwenye moja ya vyumba vilivyokuwa karibu kabisa na ofisi yake akawakaribisha na kuwaingiza ndani. Wakaingia na kukuta watoto wadogo wakiwa wamelala kwenye vitanda na wafanyakazi wachache wakiwa hapo kuwaangalia.
Hapo walitaka kuchagua mtoto mmoja tu ambaye ndiye wangemchukua na kwenda kumtunza mpaka mwisho wa uhai wake, wakafumbua macho yao yote kuwaangalia watoto hao kwa kweli walikuwa wazuri mno.
“Mnachagua mmoja tu,” sista mkuu aliongea akitabasamu.
“Mh! Watoto wote wazuri sijui tumchukue yupi kati yao?” Lina alimuuliza Phillip.
“Huyu hapa anafanana na sisi.”
“Sawa…sista huyu ndiye tuliyemchagua.”
Aliongea Phillip akimnyanyua mtoto mzuri aliyekuwa amelala kitandani, alikuwa ni mdogo lakini uzuri wake ulionekana wazi.
Upande wa pili wa hadithi hii tunamwona tajiri Fedorov akiwa hospitali ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi na tayari mtoto mmoja ameshaanza kuonyesha dalili ya kurejewa na fahamu zake kwa kupiga chafya, madaktari na wauguzi wanafurahia hilo na kuwekeza tumaini kwa mtoto mwingine wakiamini kwamba baada ya muda si mrefu naye ataamka.
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…
MAMBO hayakuwa kama walivyotarajia kwamba baada ya saa kadhaa mtoto huyo angeamka na kuungana na mwenzake, saa ya kwanza ikapita na sasa ilikuwa ikielekea ya pili, Victor Fedorov uvumilivu ukaanza kumshinda akajikuta akimwaga machozi kama mtoto mdogo, kazi ya wauguzi ndani ya chumba ikawa ni kumtuliza wakimtaka awe mvumilivu.
“Lakini ni muda mrefu sana mbona mwenzake amesharejewa na fahamu?” aliuliza akisogea karibu kabisa na kitanda cha pacha ambaye hakuonyesha dalili yoyote ya kuamka.
“Ataamka, kuwa mvumilivu.”
“Mbona kama ni upasuaji umefanyika kwa saa sawa iweje yule aamke na huyu bado?” bado aliendelea kuuliza maswali mfululizo.
“Tafadhali tunaomba sasa mzee utupishe tuendelee na matibabu yetu tutakuwa tukikujulisha kila kitu kadiri muda unavyokwenda tunaomba uende nje,” aliongea daktari mmoja, muuguzi aliyekuwa karibu na Fedorov akamshika mkono na kumwongoza kutoka nje naye pia akijaribu kuongea maneno ya kumpa faraja.
Mzee huyo akatoka akilia, mawazo na akili zake zote zilikuwa juu ya mtoto wake huyo ambaye hakuonyesha matumaini, akatembea hatua ya kwanza na ya pili kisha akageuka nyuma kuangalia mlango wa chumba cha wagonjwa mahututi.
“Sitakwenda popote nitakaa hapahapa mpaka mwisho nataka kujua nini kinaendelea,” aliongea Fedorov akiketi chini, akiwa hapo haikupita hata sekunde tatu mlinzi wake naye akaungana naye, pia akijaribu kumfariji mzee huyo lakini zoezi hilo lilionekana kuwa gumu.
“Naumia, moyo wangu una wasiwasi mkubwa sana juu ya mtoto wangu…sijui kama ataamka…lakini kama kuna kitu kibaya kwa nini wanifiche? Nataka wanieleze ukweli ili nijiandae kwa tatizo linalokuja,” aliongea akibubujikwa machozi.
“Hapana bosi hawezi kufa, Mungu mkubwa anatenda.”
“Najua hilo lakini kwa sasa nimekata…….”
“Hutakiwi kukata tamaa unachotakiwa kufanya hivi sasa ni kuamini kwamba naye pia ataamka, mimi ninaamini kwamba yuko katika mikono ya madaktari bingwa atapona tu.”
“Mh! Labda hebu tuone,”aliongea Fedorov akijifuta machozi.
***
“Mnachagua mmoja tu,” sista mkuu aliongea akitabasamu.
“Mh! Watoto wote wazuri sijui tuchukue yupi kati yao,” Lina alimuuliza Phillip.
“Huyu hapa anafanana na sisi.”
“Sawa…sista huyu ndiye tuliyemchagua.”
Mabusu mfululizo yakatua kwenye paji la mtoto waliyemchukua, alikuwa ni mtoto wa jinsi ya kike, pamoja na kuwa mtoto mdogo uzuri wake ulionekana wazi, rangi ya ngozi yake ilifanana kabisa na ya Phillip, furaha ya ajabu ikatawala, hakuwepo hata mtu mmoja kati yao aliyeamini kwamba sasa wangekuwa wakiitwa baba na mama wa mtoto waliyemuasili kutoka katika Kituo cha Msimbazi.
“Tutamlea na kumtunza mpaka mwisho wa uhai wetu tukimpatia kila aina ya mahitaji,” Phillip aliongea akimwangalia sista mkuu.
“Ombi letu kwenu ninyi ni hili hapa,” sista aliongea.
“Ndiyo sista tunakusiliza.”
“Tutakuwa tukihitaji kumtembelea mtoto huyu kila baada ya mwezi mmoja kujua na kufahamu anaendeleaje, hiyo ni moja ya sheria zetu mpaka atakapofikisha umri wa miaka kumi na nane ambapo tutakuwa huru kumwacha aendelee na maisha yake kwani atakuwa ni mtu mzima.”
“Hilo halina shaka sista na kama inawezekana tunaweza tu kuongozana mpaka nyumbani.”
“Nitawapa mtu ambaye mtaongozana naye mpaka huko kwa ajili ya kupafahamu na kama kutatokea mabadiliko yoyote yawe ya kuhama nyumba au kwenda nje ya nchi ni vyema mkatujulisha mapema, sawa?” sista mkuu aliuliza.
“Tumesikia,” Phillip na Lina walijibu kwa pamoja na kuanza kutoka nje ya chumba kuelekea ofisini kwa sista mkuu ambako wangekamilisha taratibu zote kisha kuondoka na mtoto waliyekuwa naye.
Taratibu maalum zikafanyika ikiwa ni pamoja na kupigwa picha na kutia saini kwenye makubaliano yote yaliyofanyika ofisini kisha wakakabidhiwa mtoto na sista mmoja ambaye wangeongozana naye mpaka mahali wanapoishi. Wakatoka na kumshukuru sista kisha kutembea kuelekea sehemu waliyokuwa wameegesha gari, Phillip ndiye alikuwa dereva na Lina aliketi kiti cha nyuma akiwa amempakata mtoto.
Gari liliendeshwa na kwa muda wa saa moja tu walifika nyumbani kwa Phillip na Lina wakamkaribisha sista waliyeongozana naye wakimweleza wazi kwamba hapo ndipo palikuwa nyumbani kwao ambako mtoto waliyekuwa wamemwasili angeishi maisha yake yote akitunzwa na kulelewa vyema.
“Karibu sana sista hapa ndipo nyumbani kwetu ambako mtoto huyu atalelewa na kuishi, akitunzwa kwa hali na mali.”
“Mh! Ahsanteni sana nafurahi kupafahamu tutakuwa tukija kila mwezi kumtembelea ili kujua maendeleo yake.”
“Karibuni sana.”
Dakika kumi na tano baadaye sista aliyeongozana na Phillip na Lina aliaga na kuondoka akiahidi kurejea tena baada ya mwezi mmoja kujua hali ya mtoto huyo. Wakamsindikiza kisha akaondoka.
Kwa siku nzima walishinda ndani ya nyumba wakipanga mipango yote na jinsi ya kumlea na kumtunza mtoto huyo. Lina akatoa wazo kwamba ni vyema wangemtafuta mfanyakazi wa ndani ambaye angekuwa tayari kumlea mtoto huyo na wao wangemlipa mshahara ambao angeutaka.
“Ni lazima atafutwe mtu wa kumlea mtoto huyu kwa upendo wote,” Lina aliongea.
“Kabisa, lakini nashauri awe mtu mzima kidogo.”
“Jinsi ya kumpata sasa ndiyo tatizo, sijui tuanzie wapi?”
“Hebu subiri kidogo,” Phillip aliongea akinyanyuka kitini kuelekea chumbani.
Je, nini kitaendelea? Fuatilia siku ya Jumatatu katika Gazeti la Ijumaa Wikienda.
Comment
Good story
Comment by HAPPINESS MARCEL MASSAWE on February 10, 2012 at 9:31pm Mh. kazi ipo hapo kwenye kumlea huyo mtoto
mnatakiwa kutafunta mtu anayependa watoto la sivyo mtaumbuka
Comment by Daudi on February 10, 2012 at 9:09pm Huyo yaya asijekuwa ndio mama wamtoto alimtelekeza kwa sbb ya ugumu wa maisha.
Comment by Van Lusiu on February 10, 2012 at 8:15pm
Comment by kaka on February 10, 2012 at 2:24pm MMMMMMMMEEEE TEEEEEEE
Comment by laurenciamsunga on February 10, 2012 at 1:14pm
Comment by FURAHA TAUSI on February 10, 2012 at 11:01am EHE
| 1 |
GLOBAL |
| 2 |
julius manning |
| 3 |
Man KKK |
| 4 |
Sili Silali |
| 5 |
IL-YA |
| 6 |
chama baby |
| 7 |
msichoke mlugu |
| 8 |
kaka |
| 9 |
Maji Marefu |
| 10 |
Kelvin Luhala Eto'o |
othman Ochu posted a status
mrembo commented on Sili Silali's photo

You need to be a member of Global Publishers to add comments!
Join Global Publishers