Queen of the Gorillas (Malkia wa Masokwe) - 59

MAISHA ya familia ya Dk Lewis yanarudi kwenye mstari na anafanikiwa kuiunganisha upya familia yake kufuatia kupatikana kwa mtoto wake wa kipekee, Skyler ambaye alitoweka kipindi kirefu kilichopita. Skyler anakuja  na mtoto wa kiume, Harrison ambaye amefanana vitu vingi na marehemu baba yake.
Siku zinasonga mbele kwa kasi na Harrison anazidi kuwa mkubwa. Anamaliza elimu ya msingi na kuanza shule ya sekondari anakohitimu kidato cha nne. Baadaye anajiunga na chuo cha Michigan State University anakosomea masomo ya tabia za wanyama, Ethology. Anahitimu masomo yake na kuwa mtaalamu wa tabia za wanyama.
Baada ya kuhitimu masomo, anaenda kufanya utafiti kwenye msitu wa Tongass, lengo lake likiwa ni kujua mambo mbalimbali yahusuyo wanyama, hususan sokwe wengi wanaopatikana kwenye msitu huo mkubwa.
Je, nini kitafuatia?
SONGA NAYO...
ILIBIDI akajibanze kwenye mti mkubwa na kuangalia ni wanyama gani, macho yake yakatua kwenye kundi kubwa la sokwe wakubwa waliokuwa wanaruka kutoka tawi moja kwenda jingine kwa kasi kubwa, wakawa wanaelekea pale alipokuwa amejibanza.
Kelele zilizidi kuongezeka, utulivu uliokuwepo ndani ya msitu ule ukatoweka, Harrison akazidi kujibanza pale kwenye mti huku bastola yake iliyokuwa inatumia risasi za mpira ikiwa mkononi, tayari kwa kujihami endapo lolote lingetokea.
“Mungu wangu, mbona wakubwa hivi? Halafu mbona wengi kiasi hiki?” alijiuliza Harrison huku akiichukua kamera yake kwenye begi kwa mkono mmoja, akakaa vizuri na kuanza kupiga picha kwa mbali. Alipiga picha kadhaa, akawa anaendelea kushangaa jinsi sokwe wale walivyokuwa wakubwa na wengi.
Kundi lile la masokwe lilipotoweka, alishusha pumzi ndefu na kuweka vifaa vyake vizuri. Ilibidi arudi kwenye hema lake, akaenda kuweka kumbukumbu za alichokiona. Akawa anaandika baadhi ya mambo kwenye kijitabu chake cha kumbukumbu.
Siku zilizidi kuyoyoma Harrison akiwa bado ndani ya msitu wa Tongass, kila siku akawa anaendelea na kazi ya utafiti juu ya tabia za masokwe na viumbe wengine katika msitu ule, pamoja na kuchunguza uoto wa asili. Taratibu alianza kuwazoea masokwe wale wakubwa na wa kutisha.
Tofauti na wanyama wengine, sokwe wa msitu wa Tongass walikuwa wakitembea kwa makundi makubwamakubwa, huku moja likionekana kuwa kubwa zaidi. Kila alipobahatika kuwaona, walikuwa kwenye makundi, wakiruka juu ya matawi ya miti kwa namna ambayo ilimshangaza sana Harrison.
Baada ya kukaa kwa muda wa wiki mbili ndani ya msitu ule, Harrison aliamua kuondoka na kurejea nyumbani kwao kwenda kufanyia kazi taarifa mbalimbali za kiuchunguzi juu ya tabia za wanyama hususan masokwe wa Msitu wa Tongass alizozipata.
Alijiandaa kwa kufungasha vitu vyake vyote, akalikunjua hema na kulibana kwa namna ambayo ilikuwa rahisi kubebeka, alipohakikisha amechukua kila kitu, aliianza safari ya kuelekea kwenye ofisi za msitu ule kwa ajili ya kukabidhi baadhi ya vifaa alivyokuwa amepewa.
“Umefanikiwa?”
“Nimefanikiwa kwa kiasi kikubwa na namshukuru Mungu sijapata madhara yoyote.”
“Unawaonaje masokwe wa Msitu wa Tongass?”
“Mh! Sijawahi kuona sokwe wakubwa kama hawa, halafu wanatembea kwa makundi makubwa sana, lazima nitarudi tena kwani nadhani ndani ya msitu huu nitajifunza vitu vingi ambavyo awali sikuwa navifahamu.
“Ngoja nikafanyie kazi hizi data nilizozipata,” alisema Harrison wakati akizungumza na askari wa wanyama pori aliyemkuta kwenye ofisi za msitu ule.
Baada ya makabidhiano, Harrison alitembea kwa miguu kwa kilometa chache kabla ya kuifikia barabara kuu. Akasimamisha gari na safari ya kurejea nyumbani kwao, Miami ikaanza.
”Ooh! Karibu baba, umekuwa mweusi kweli, inaonesha kuna baridi sana huko ulikotoka.”
“Ahsante sana, kuna baridi kali kwenye Msitu wa Tongass lakini namshukuru Mungu nimefanikiwa kwa kiasi kikubwa,” alisema Harrison wakati akipokelewa na bibi yake.
“Mama yupo wapi?”
“Ameenda kazini lakini muda si mrefu atarudi. Mh! Habari za huko?”
“Nzuri kabisa mama, nimeifurahia sana safari yangu kwenye Msitu wa Tongass, nimewaona sokwe wakubwa haooo! Yaani hata wewe nikikuonesha picha utashangaa,” alisema Harrison.
Baada ya kuingia ndani na kupumzika kwa muda, Harrison alienda kuoga na kubadilisha nguo, akachukua kamera zake mbili alizokuwa anazitumia kupigia picha na kwenda kuziunganisha kwenye kompyuta kwa lengo la kuzitoa zile picha na kuzihifadhi vizuri.
Alichomeka waya maalum kutoka kwenye kamera na kuunganisha kwenye kompyuta, akaanza kutoa picha, zoezi lililomchukua zaidi ya nusu saa. Alipomaliza alianza kuzichunguza vizuri moja baada ya nyingine. Aliendelea na zoezi lile huku akizitenganisha katika mafaili mbalimbali, kuanzia zile za mazingira, za uoto wa asili mpaka zile za makundi ya sokwe.
Wakati akiendelea kuzifuatilia, aligundua jambo ambalo lilimshangaza. Kila alipokuwa akizichunguza kwa makini picha alizopiga makundi yale ya sokwe, aligundua kama kuna kitu katikati yao ambacho hakikuwa kikionekana vizuri.
Alibaini pia kuwa sokwe wale walikuwa wakitembea kwa mtindo wa kuweka duara, hata walipokuwa wanaruka kutoka mti mmoja kwenda mwingine, katikati kulikuwa na kitu ambacho walionekana kukilinda kwa nguvu kubwa.
“Hiki ni nini?” alisema Harrison huku akijaribu kuivuta picha karibu kwenye kompyuta, ‘akai-zoom’ mpaka mwisho, hali iliyomsaidia kuona vizuri, akagundua kuna kitu kilikuwa katikati ya sokwe wale ingawa hakuelewa mara moja ni kitu gani.
Aliendelea kufuatilia picha zile kwa muda, akajikuta akisisimka mwili mzima kutokana na kitu alichokuwa anakiona.
“Lazima nirudi Tongass, nitaenda kufuatilia kwa makini ili nijue ni kitu gani,” alijisemea Harrison huku akiendelea kuzitazama zile picha. Aliifanya kazi ile kwa muda mrefu mpaka muda wa kulala ulipowadia.
Kesho yake, alfajiri na mapema Harrison aliamka na kuaga kuwa anarudi tena kwenye msitu wa Tongass kuendelea na kazi.
“Wewe si ulisema utapumzika kidogo? Kinachokufanya uwahi kurudi bila kukaa nasi hata kidogo ni nini?”
“Mama kuna kazi ya muhimu nilikuwa sijaimalizia, ni muhimu sana,” alisema Harrison bila kutaka kufafanua ni kazi gani. Mama yake hakuwa na hiyana, alimruhusu lakini akawa anajiuliza maswali mengi ambayo hayakupata majibu.
Harrison akasafiri kwa mara nyingine kurudi kwenye msitu wa Tongass. Safari hii hakupanda treni bali alisafiri kwa mabasi, akaunganisha safari mpaka alipofika Tongass.
“Mbona umerudi tena? Kuna kitu umesahau?” askari wa wanyama pori aliyemuacha jana yake, alimuuliza Harrison, akamweleza kuwa kuna jambo la muhimu alisahau kulifanyia kazi. Hata hivyo, hakumueleza ni jambo gani, akapewa vifaa na kurudi msituni, akaenda kuweka kambi pembeni kidogo ya pale alipokuwa amesimamisha hema lake.
Kwa kuwa tayari muda ulikuwa umeenda huku uchovu wa kuunganisha safari ukimsumbua, Harrison aliamua kupumzika mpaka kesho yake. Kulipopambazuka tu, aliwahi kuamka na kwenda nje ya hema, akawa anaangaza macho huku na kule akitegemea kuliona tena lile kundi la sokwe.
Muda ulianza kwenda lakini masokwe hawakutokea, ikabidi aanze kuwatafuta sehemu mbalimbali za msitu ule. Kuna wakati alisikia kelele, akahisi watakuwa ni wenyewe lakini alipofuatilia, alikuta kundi la tai likiufaidi mzoga wa mnyama aliyekuwa amejifia.
Akaendelea kuzunguka huku na kule, akijipenyeza katikati ya miti iliyokuwa imefungamana  ndani ya msitu huo. Baada ya kuhangaika sana bila mafanikio, Harrison aliamua kurudi kwenye hema lake kupumzika. Akiwa mita chache kutoka kwenye hema, alianza kusikia kelele upya, alipoangaza macho yake juu ya miti, aliwaona sokwe wakiruka kwa kasi, akatafuta sehemu na kujibanza, akawa anaangalia kwa makini katikati ya lile kundi.
Kamera yake nayo ilikuwa mkononi, akiwa tayari kupiga picha endapo angekiona kile kitu alichokuwa anakisubiri. Hata hivyo, kazi haikuwa nyepesi, kila sokwe wale walipokuwa wanaruka, walikuwa wameweka duara huku wakiwa makini kuziba kitu kilichokuwa katikati yao.
Je, nini kitafuatia? Usikose kufuatilia Ijumaa kwenye Gazeti la Ijumaa.

Views: 1784

Tags: hadithi11

Comment

You need to be a member of Global Publishers to add comments!

Join Global Publishers

Comment by raphael Joram on November 20, 2012 at 4:09pm
mh!yule mtoto
Comment by DORAH FREDY on November 20, 2012 at 11:33am

Hicho kitu ni yule mtoto wa Doctor ha ha ah ha ah haaa

Comment by Nadra M. Issa on November 19, 2012 at 4:32pm
hahaha icho kitu ni yule mtoto quen of gorillas
Comment by FURAHA TAUSI on November 19, 2012 at 4:29pm
mmmmh makubwa sasa hayo mimi ningekimbia nivunjike naogopa sana hao wadudu
Comment by Richard Rugajo on November 19, 2012 at 1:30pm

Hadithi tamu sana hii, yaani mhh! asante kaka!!

Comment by SAIDI ABDUL SAID on November 19, 2012 at 11:34am

nimeipienda sana iyo big up sana

ADVERTISEMENT


Advertisement

 

Forum

KIPIGO CHA BAO 2-1 KWA MAN UTD, KOSA LA MWAMUZI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Mohammed Mar 26. 6 Replies

JE, NI KWELI KWAMBA KIPIGO CHA BAO 2-1 ILICHOKIPATA MAN UTD KUTOKA KWA REAL MADRID USIKU WA KUAMKIA LEO LAWAMA ZOTE ZIMWENDEE MWAMUZI WA MCHEZO AU MAN UTD WAJILAUMU WENYEWE? TUPE MAONI YAKO!!!

HALI INAYOENDELEA BUNGENI, SPIKA NA NAIBU WAKE WAMESHINDWA KUONGOZA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Ali Abdalla Ali Apr 22. 20 Replies

Tumeshuhudia kwa siku za hivi karibuni hali halisi iliyokuwa inatokea katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, kwa hali hii ni ishara kuwa Spika na Naibu wake washindwa kuliongoza bunge hilo?

VURUGU ZA CCM NA CHADEMA KUGOMBEA MLINGOTI WA BENDERA DODOMA, NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Phinehas Rishiansia Kileo May 3. 6 Replies

Wafuasi wa CCM wakimshambulia mfuasi wa Chadema mkoani Dodoma…

Tags: BENDERA, WA, DODOMA, NANI, KULAUMIWA?

VURUGU ZINAZOENDELEA HAPA NCHINI NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by NELSON UVAMBE on Monday. 27 Replies

HIVI KARIBUNI KUMEKUWEPO UPOTEVU WA AMANI HAPA NCHINI PAMOJA NA WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI. MKOANI KAGERA WANANCHI WENYE HASIRA WALIWAUA POLISI, IJUMAA ILIYOPITA WAKULIMA NA WAFUGAJI HUKO WILAYANI KILOSA WALIZUA VURUGU NA KUFUNGA BARABARA,…

MRISHO NGASSA KUPELEKWA SIMBA SC BILA RIDHAA YAKE, JE NI HALALI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Domino Bagambisa Jan 21. 17 Replies

Kiungo hatari wa Azam FC, Mrisho Ngassa leo amepelekwa Simba SC kwa mkopo na timu yake…

Tags: SOKA

hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Started by Gysper in Siasa. Last reply by Jamal amor May 9. 24 Replies

 hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Kauli Ya JK kuwa Mauaji ya Arusha ni "Bahati Mbaya"

Started by Kulikoni Ughaibuni in Siasa. Last reply by richardngeze Feb 12. 12 Replies

Tanzania tuna tatizo kubwa.Hakuna haja ya kunyoosheana vidole as to nani amechangia tatizo hilo bali cha muhimu na haraka ni namna tutakavyoweza kutatua tatizo hili.Nisimung'unye maneno: tatizo kubwa linaloikabili ni kuwa na Rais ambaye takriban…

Latest Activity

nyakisimbo shamawele posted a status
"DUNIA HII INA MAMBO MENGI !!!!"
9 minutes ago
FURAHA TAUSI commented on GLOBAL's blog post WOLPER, BABY MADAHA BIFU LA KIFO!
"wasanii mna mambo nyie?"
15 minutes ago
FURAHA TAUSI commented on GLOBAL's blog post NIYONZIMA ASAINI YANGA MIAKA 2
"manji ni noma..."
15 minutes ago
LJH_3 commented on GLOBAL's blog post KAMA UNATAKA FURAHA, FUATA MTINDO HUU WA MAISHA!
"Naona mkeo ana raha sana kupata mume kama wewe..."
15 minutes ago
LJH_3 commented on GLOBAL's blog post BUNGENI NGUMI NJENJE!
"Yaani sipati picha kabisa hapo...kilichobaki kila mmalizapo vikao tafuteni ulingo muingie kwenye…"
15 minutes ago
LJH_3 commented on GLOBAL's blog post FLORA, H- BABA NDOA SASA NI JUNE 8
"Kwahiyo H-Baba alikuwa anangoja aone kama una mbegu za kuzalishwa ndio ameamua kukuoa kwanini…"
15 minutes ago
BEN BENO commented on GLOBAL's blog post Kibadeni kuanza kuinoa Simba Mei 28
"Timua Timua mpaka lini jaman simba? Embu achen hizo."
15 minutes ago
LJH_3 commented on GLOBAL's blog post NIYONZIMA ASAINI YANGA MIAKA 2
"Hope dua la kuku hilo.. na kelele za chura hazimzuii ng'ombe kunywa maji..Niyo ulichoamua ni…"
15 minutes ago
kulthum mattar commented on GLOBAL's blog post THE DIRTY GAME (MCHEZO MCHAFU) - 13
"na huyo siku yake imefikaaa maliza wote haoo mbwa poriiii"
15 minutes ago
kulthum mattar commented on GLOBAL's blog post Queen of the Gorillas (Malkia wa Masokwe) - 113
"zaidi ya gaidi linda acha roho mbaya hiyo nawe mwnamke utaolewa na kuzaa ujue uchungu wa mwana "
15 minutes ago
kulthum mattar commented on GLOBAL's blog post THE SECRET AGREEMENT - 12
"haya tenaaa kazi za majini hizo huwa hawataniwi haooo malizana naeeee"
15 minutes ago
FURAHA TAUSI commented on GLOBAL's blog post RAMA MLA WATU, MAMA YAKE WAACHIWA NA MAHAKAMA
"mmmh!!!! sasa huko mahabusu mbona hakuwa anakula watu kama ni kichaa??? kweli duniani hakuna haki"
16 minutes ago

© 2013   Created by Global Publishers.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service