MUME AMLIPUA KWA MOTO MKEWE, KISA WIVU

MWANAMKE aliyefahamika kwa jina la Subira Malefya (53), mkazi wa Kijiji cha Ipinda wilayani Kyela, mkoani hapa, amelazwa katika hospitali ya wilaya baada ya kumwagiwa mafuta ya taa na kuchomwa moto na mumewe ambaye ni mwalimu mstaafu, Boniface Mwakinyuke (64).

Kaimu Katibu Tarafa wa Ntebela, Cathbert Mwalukama alisema kuwa mwanamke huyo alimwagiwa mafuta ya taa mwili mzima kisha kuchomwa moto saa nne usiku hivi karibuni akiwa amelala fofofo.

“Siku hiyo walikuwa wote kwenye kilabu cha pombe lakini mke aliwahi kurudi nyumbani na alilala,” alisema Mwalikama.

Hata hivyo, baadhi ya watu waliokuwa kilabuni walioogopa kutaja majina walisema mwalimu huyo mstaafu alipoona mkewe kaondoka alianza ‘kulia’ wivu kwamba  amechukuliwa na mwanaume mwingine.

Walisema mwalimu huyo baadaye alikwenda dukani na kununua mafuta ya taa lita moja na nusu na kiberiti na kwenda nayo nyumbani kwake ambapo aliyatumia kumlipua mkewe.

Baada ya kitendo hicho, wasamaria walimkimbiza mama huyo katika Kituo cha Afya cha Ipinda na baadaye akahamishiwa Hospitali ya Wilaya ya Kyela ambapo anaendelea na matibabu. Mwalimu huyo alikamatwa na kufikishwa Kituo cha Polisi Kyela ambako anashikiliwa.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Kyela, Dk. Festo Ndungange amethibitisha kumpokea mgonjwa huyo na kusema amelazwa wadi namba tatu kwa matibabu zaidi.

Views: 793

Tags: amani11

Comment

You need to be a member of Global Publishers to add comments!

Join Global Publishers

Comment by edista joshua on October 25, 2012 at 4:23pm

jamani wivu hadi uzeeni

Comment by Berthaa Kobelo on October 25, 2012 at 1:24pm

we babu huoni kuwa umri wako na mambo uliyoyafanya hayaendani!!!!!!!!!!!..sa km ulihisi wivu kwann usingeenda na mkeo nyumbani!!!!..yn elimu iliyonayo nadhani haikusaidia kitu..sasa km angekufa je..nae siungefia jela na huo umri wako jamani..mbona unambipu Isarael!!!!!!!!

ADVERTISEMENT


Advertisement

 

Forum

KIPIGO CHA BAO 2-1 KWA MAN UTD, KOSA LA MWAMUZI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Mohammed Mar 26. 6 Replies

JE, NI KWELI KWAMBA KIPIGO CHA BAO 2-1 ILICHOKIPATA MAN UTD KUTOKA KWA REAL MADRID USIKU WA KUAMKIA LEO LAWAMA ZOTE ZIMWENDEE MWAMUZI WA MCHEZO AU MAN UTD WAJILAUMU WENYEWE? TUPE MAONI YAKO!!!

HALI INAYOENDELEA BUNGENI, SPIKA NA NAIBU WAKE WAMESHINDWA KUONGOZA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Ali Abdalla Ali Apr 22. 20 Replies

Tumeshuhudia kwa siku za hivi karibuni hali halisi iliyokuwa inatokea katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, kwa hali hii ni ishara kuwa Spika na Naibu wake washindwa kuliongoza bunge hilo?

VURUGU ZA CCM NA CHADEMA KUGOMBEA MLINGOTI WA BENDERA DODOMA, NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Phinehas Rishiansia Kileo May 3. 6 Replies

Wafuasi wa CCM wakimshambulia mfuasi wa Chadema mkoani Dodoma…

Tags: BENDERA, WA, DODOMA, NANI, KULAUMIWA?

VURUGU ZINAZOENDELEA HAPA NCHINI NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by mayalilwa Mar 8. 26 Replies

HIVI KARIBUNI KUMEKUWEPO UPOTEVU WA AMANI HAPA NCHINI PAMOJA NA WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI. MKOANI KAGERA WANANCHI WENYE HASIRA WALIWAUA POLISI, IJUMAA ILIYOPITA WAKULIMA NA WAFUGAJI HUKO WILAYANI KILOSA WALIZUA VURUGU NA KUFUNGA BARABARA,…

MRISHO NGASSA KUPELEKWA SIMBA SC BILA RIDHAA YAKE, JE NI HALALI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Domino Bagambisa Jan 21. 17 Replies

Kiungo hatari wa Azam FC, Mrisho Ngassa leo amepelekwa Simba SC kwa mkopo na timu yake…

Tags: SOKA

hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Started by Gysper in Siasa. Last reply by Jamal amor May 9. 24 Replies

 hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Kauli Ya JK kuwa Mauaji ya Arusha ni "Bahati Mbaya"

Started by Kulikoni Ughaibuni in Siasa. Last reply by richardngeze Feb 12. 12 Replies

Tanzania tuna tatizo kubwa.Hakuna haja ya kunyoosheana vidole as to nani amechangia tatizo hilo bali cha muhimu na haraka ni namna tutakavyoweza kutatua tatizo hili.Nisimung'unye maneno: tatizo kubwa linaloikabili ni kuwa na Rais ambaye takriban…

Latest Activity

© 2013   Created by Global Publishers.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service