Mtoto Cesilia Edward enzi za uhai wake.

Mtoto Cesilia Edward amefariki dunia juzi saa tano usiku wa tarehe 08 katika hospitali ya Regency ya hapa jijini Dar es Salaam ambapo alikuwa amelazwa kwa siku mbili kwaajili ya matibabu.
Marehemu Cesilia alikuwa na umri wa miaka 14 alikuwa na tatizo la moyo na figo kushindwa kufanya kazi na kusababisha tumbo kujaa maji na kuvimba. Aligundulika na tatizo hilo tangu alipozaliwa.
Kampuni ya Africa media Group wamiliki wa Channel ten Kupitia kipindi mimi na Tanzania ilifanikiwa kumpeleka mtoto Cesilia nchini India kwa matibabu mwaka 2011 mwezi Oktoba lakini hakufanikiwa kupata matibabu (operation) baada ya madaktari kuthibitisha kuwa alikuwa amechelewa kwa matibabu.
Cesilia alikuwa mtoto yatima na kulelewa na familia ya Bw. Peter Nyarugembe mkazi wa Mbagara kuu ambaye alikuwa akimlea baada ya kukuta akilelewa na dada yake wilayani Kisarawe na alimkuta na tatizo hilo ila kutokana na hali ya uchumi aliyo nayo hakuweza kumsaidia kupona ugonjwa alio nao na kuamua kuomba msaada kwa wasamalia wema kupitia Kipindi cha mimi na Tanzania.
Marehemu alifikishwa hospitali jumatatu ya tarehe 6 mwezi huu akiwa na hali mbaya iliopelekea kupoteza fahamu na kumbukumbu kila wakati hali iliendelea hivyo mpaka umauti ulipo mkuta.
Mungu ailaze roho ya marehemu Cesilia mahala pema peponi.

-Amen.

Views: 1538

Tags: AFARIKI, CESILIA, DUNIA, EDWARD, MTOTO

Comment

You need to be a member of Global Publishers to add comments!

Join Global Publishers

Comment by Santa Santiago on February 16, 2012 at 10:21am

R.I.P CECY

Comment by mawnaisha bakary vuyaa on February 13, 2012 at 12:11pm

mungu ailaze pema peponi roho ya marehemu Cecilia

Comment by Neema Kibwana Shomary on February 13, 2012 at 10:25am
R.I.P CECILIA
Comment by ANDERSON SOGOLE on February 13, 2012 at 8:28am
huu ugonjwa nao eeeh, hujafa hujaumbika
Comment by samora rajab albert on February 11, 2012 at 7:50pm

innaa lillahi wainna ilayhi rajiun

Comment by Kakytee The Director on February 11, 2012 at 8:59am
Inna lillahi wainna ilayhi raajiuun, mungu ailaze roho yake mahali pema
. Aamin pumzika kwa amani mpenzi cecilia, mungu pia aipe subra familia ya waliomlea, a$ well as mdada HOYCE TEMU kwa jitiihada zako.
Comment by kokusima on February 10, 2012 at 11:45pm
Jamani imeniuma, niliskitika sana aliporudi toka india akidaiwa sumu alokula ilikuwa imedhazagaa kwa hiyo alicjelewa. Jamani serikali yetu ni yatajiri tu? Sisi yatima na maskini tufe tu kwasababu hatuna kitu, lini serikali yetu itaamka lakini?? Ee Mwenyezi Mungu mpe nafasi njema mwanao na uzidi kuimlika nchi yetu, utuondolee watafuna nchi na utupe viongozi bora. Tanzania inamalizwa na wenye meno. Mungu mbariku Hoyce Tem kwa kazi nzuri aliyoifanya na anayoendelea kuifanya. Mungu ni mwema.

R.I.P mtoto Cecy
Comment by MARIA ROSSA on February 10, 2012 at 9:49pm

Poleni sana familia. Pumzika kwa amani mtoto mwema usiye na hatia Cecy.

Comment by julius manning on February 10, 2012 at 4:57pm

poleni sana wana familia. Mungu amweka mahali pema peopni, Amina.

Comment by Lillian j on February 10, 2012 at 4:48pm

pumzika kwa amani mpendwa we2 umeteseka sana


ADVERTISEMENT


TANGAZA HAPA

ADVERTISEMENTS

Latest Activity

GUNZ TRUVADA posted a status
"KUMPA ASIYE KUPA NI SAWA SAWA NA KUTUPA"
6 minutes ago
GUNZ TRUVADA posted a status
"KUMPA ASIYE KUPA NI SAWA SAWA NA KUTUPA"
6 minutes ago
othman Ochu posted a status
"SCENE 1 WAHUSIKA: AMIDU , SHARIFA MAHALI: ZANZIBAR MUDA : JIONI ( WAKIWA WANASHUKA TOKA KATKA BOTI YA JION KUINGIA KATKA MJI WA ZANZI"
9 hours ago
Priscus Adelard shared GLOBAL's blog post on Facebook
9 hours ago
mrembo commented on julius manning's photo
Thumbnail

Mtanzania huru

"pole sana usijali iko siku mungu atakujaalia mungu hamtupi mja wake"
10 hours ago
mrembo commented on Sili Silali's photo
Thumbnail

Duh!

"mama mzima hayawani mavazi gani hayo takupa mfano chungwa likiwa halijamenywa unatamani ulile…"
10 hours ago
kaka commented on Ali Amur Ali's video
Thumbnail

AZIMIO LA KUANGAMIZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE

"hapo ni kina dada kutua comment zao"
10 hours ago
Gaston Kayombo commented on Ali Amur Ali's video
12 hours ago
roylicious and Jackson Jacob are now friends
12 hours ago
babu wa loliondo (cup) updated their profile
12 hours ago
julius manning commented on julius manning's photo
Thumbnail

vijana 2016 itakuwa hivi

"@furaha mimi ni kikongwe hayo ni kazi kwako."
13 hours ago
Masalu Mayeji Many'hasimha shared GLOBAL's blog post on Facebook
13 hours ago

© 2012  

Designed & Developed by
G5 CLICK COMPANY.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service

How to make a Website