MGONJWA AANGUKA BARABARANI AKITOKEA HOSPITALI MORO


Joseph akiwa amelala barabarani ambako baadaye wananchi walifika na kumsaidia.

JAMAA mmoja ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Joseph, leo asubuhi alikutwa na kamera yetu akiwa ameanguka katika Barabara ya Forest mjini Morogoro, pembezoni mwa uzio wa Hospitali Kuu ya Mkoa wa Morogoro, akidai kwamba alikuwa ametokea katika hospitali hiyo na kwamba hali yake ilikuwa imezidi kuwa mbaya.

Akizungumza na mtandao huu, Joseph alisema: "Nimetoka humu ndani (hospitali) kutibiwa na baada ya kupewa dawa niliruhusiwa kurudi nyumbani, nilipofika hapa nimezidiwa na njaa pamoja na ukali wa dawa hizo na kujikuta nikiishiwa nguvu na kuanguka.

Kama kuna mtu ana shilingi elfu moja anisaidie nikanunue walau uji," alisema Joseph huku akionekana akitetemeka kwa njaa pamoja na ukali wa dawa hizo.

Alipoulizwa anasumbuliwa na ugonjwa gani alidai ni homa ya matumbo (typhoid) iliyoambatana na homa kali.

Mwandishi wetu alimpatia kiasi hicho cha fedha ambapo pia baadhi ya watu waliokuwa eneo hilo walimuunga mkono mpiga picha wetu kwa kumuongezea kiasi cha fedha na baadaye kumwinua hadi kwenye mgahawa uliopo jirani na Shule ya Sekondari ya Morogoro.

Baada ya kupata hudumu hizo, Joseph alizinduka na kauli yake ya kwanza ilikuwa ni kuushukuru mtandao huu na wananchi wengine kwa kumpatia msaada huo.



PICHA NA DUNSTAN SHEKIDELE /GPL, MOROGORO

Views: 4

Tags: AANGUKA, AKITOKEA, BARABARANI, HOSPITALI, MGONJWA, MORO

Comment

You need to be a member of Global Publishers to add comments!

Join Global Publishers

Comment by Angela Mushumbusi on December 10, 2010 at 9:34am

Pole kaka kwa yote yaliyokusibu, wa kulaumiwa ni hao madaktari jaman!!!! Asanteni sana kwa wote mliotoa msaada kwa ndugu yetu huyu make si mchezo mpaka mtu unaanguka chini, hayo mapito kaka Mungu atashusha heri, kikubwa ni uzima tuuuuu....

Comment by FURAHA TAUSI on December 10, 2010 at 8:47am

JAMANI DAKTARI MNATAKA KUUWA MBONA HAMUWEZI KUANGALIA MTU NA KUMSAIDIA???

 

POLE SANA KAKA.

Comment by rosalinda jenes on December 10, 2010 at 7:56am

Madaktari siku hizi nafikiri vyeti ni vya kuchakachua......dr anampa mgonjwa dawa bila kumwamboa masharti .....km meza dawa hizi baada ya kula...........siku hizi hawaulizi kama una alerji ya dawa wanayokupa ama vipi.......mzee magufuli ni shahidi wa udhaifu huu.......naona yeye hakuutambua, vinginevyo ninvyomfahamu mie anglivalia njuga..........siku hizi afya ya mlaji haithaminiwi ni pesa kwenda mbele...... Udumu JK

Comment by Ernest Gregory Ndunguru on December 10, 2010 at 7:30am

Sijui chama na ugonjwa wa mtu vinahusiana nini? We Jamali acha tabia ya kibaguzi haina maana. Binadamu hatukosi ya kuongea. Mliomsaidia mungu atawazidishia mara dufu.

Comment by lion on December 10, 2010 at 6:14am

pole sana Joseph hayo ni mapito bro yana mwisho kaka.

Comment by Bena Mushi on December 10, 2010 at 2:55am

Mmmh, jamani ni huruma mtu mpk njaa imemdondosha mbarikiwe sn mliomwezesha walau kwa chakula na maji.

Comment by bongo on December 10, 2010 at 2:16am

Jamani ambulance kwani Tanania hatuna uwezo wa kununua??????

Comment by DR.kim on December 9, 2010 at 5:59pm
thanks guys for ur help
Comment by jamali omary on December 9, 2010 at 4:30pm
kavaa shati la chama fulani.uchaguzi umekwisha mmeshasaulika subirini mwaka 2015


ADVERTISEMENT


TANGAZA HAPA

ADVERTISEMENTS

Latest Activity

GUNZ TRUVADA posted a status
"KUMPA ASIYE KUPA NI SAWA SAWA NA KUTUPA"
5 minutes ago
GUNZ TRUVADA posted a status
"KUMPA ASIYE KUPA NI SAWA SAWA NA KUTUPA"
5 minutes ago
othman Ochu posted a status
"SCENE 1 WAHUSIKA: AMIDU , SHARIFA MAHALI: ZANZIBAR MUDA : JIONI ( WAKIWA WANASHUKA TOKA KATKA BOTI YA JION KUINGIA KATKA MJI WA ZANZI"
9 hours ago
Priscus Adelard shared GLOBAL's blog post on Facebook
9 hours ago
mrembo commented on julius manning's photo
Thumbnail

Mtanzania huru

"pole sana usijali iko siku mungu atakujaalia mungu hamtupi mja wake"
10 hours ago
mrembo commented on Sili Silali's photo
Thumbnail

Duh!

"mama mzima hayawani mavazi gani hayo takupa mfano chungwa likiwa halijamenywa unatamani ulile…"
10 hours ago
kaka commented on Ali Amur Ali's video
Thumbnail

AZIMIO LA KUANGAMIZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE

"hapo ni kina dada kutua comment zao"
10 hours ago
Gaston Kayombo commented on Ali Amur Ali's video
12 hours ago
roylicious and Jackson Jacob are now friends
12 hours ago
babu wa loliondo (cup) updated their profile
12 hours ago
julius manning commented on julius manning's photo
Thumbnail

vijana 2016 itakuwa hivi

"@furaha mimi ni kikongwe hayo ni kazi kwako."
13 hours ago
Masalu Mayeji Many'hasimha shared GLOBAL's blog post on Facebook
13 hours ago

© 2012  

Designed & Developed by
G5 CLICK COMPANY.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service

How to make a Website