Maulidi Kitenge aoa mke wa tatu

Prizenta anayekimbiza kwenye habari za michezo na burudani Bongo, Maulidi Baraka Kitenge amevuta mke wa tatu, Ijumaa limepenyezewa.

Kwa mujibu wa sosi wa habari hii ambaye jina lake linawekwa kibindoni kwa sasa, Maulidi ‘Namba Tisa Mgongoni’, amefunga ndoa na Mwanaidi Yatery Juni 17, 2010 kwenye Msikiti wa Kichangani, Magomeni Mapipa jijini Dar.
Ikazidi kuanikwa kwamba, baada ya ndoa hiyo, cherekochereko na vifijo vilihamia nyumbani kwa wazazi wa Bibiharusi, Mabibo, Dar.

Aidha, Juni 20, 2010 kukafanyika Maulidi kwenye ukumbi uliopo jengo la May Fair, Mikocheni, Jijini Dar kabla ya kufunga pazia kwa Pati ya ‘kuvunja na shoka’ iliyotwaa nafasi yake Jumamosi ya Juni 26, 2010 ndani ya hoteli ya Paradise, iliyopo Jengo la Benjamin Mkapa, Barabara ya Azikiwe, jijini Dar.


Wakati huo huo habari zisizo na chenga zinasema kuwa, mtangazaji huyo ameamua kufunga ndoa na Mwanaidi baada ya kumpiga chini kwa talaka aliyekuwa mkewe wa pili Januari mwaka huu.

“Unajua kwanini jamaa kaamua kuoa mke mwingine? Yule aliyemuoa mwaka 2007 alimpa talaka Januari mwaka huu, kwa hiyo nafasi ikabaki tupu,” kilisema chanzo chetu.
Juhudi za kumpata Maulidi ziligonga mwamba baada ya simu yake ya mkononi kuita kwa muda mrefu bila kupokelewa hata pale iliporudiwa.

Hata hivyo, mtu wake wa karibu alipopatika na kuulizwa alithibitisha kuwepo kwa ndoa hiyo na pia alikiri kuwepo kwa talaka kwa mke wa pili, Rehema Kayugwa, hivyo kumfanya mtangazaji huyo kuendelea kuwa na wake wawili licha ya kufunga ndoa ya tatu. Mke mkubwa wa Maulidi anaitwa Eshe Muhidin ambaye pia ni mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha TBC1.

Gazeti hili linamtakia maisha mema ndani ya ndoa mpya huku akikumbuka kuwa, mke ndani ya nyumba hapigwi kwa fimbo au makofi, hupigwa kwa upande wa khanga.

Views: 1573

Tags: ijumaa11

Comment

You need to be a member of Global Publishers to add comments!

Join Global Publishers

Comment by hajimakame on February 3, 2011 at 10:49am
 nyinyi akina dada hivi upi ni umalaya  kati ya nyumba ndogo au kuoa wake watatu tambueni idadi ya wasichana  mara tano zaidi ya wavulana. sasa nani atakayewaoa hawa dada zetu katika idadi kama hiyo .kuoa mke mmoja ni kujiweka katika risk ya kupata maambukizo ya virusi vya ukimwi, maana ukiwa na wake zaidi ya mmoja ni kuwasitiriana . mwachieni aoe 1,2,3, mpaka 4 sasa kuoa uzeeni ndio atakua hawamudu sasa ndio anawamudu kwa sababu ana nguvu uwezo wa kuwahudumia  akioa wakatiwa uzeeni hataweza kutekeleza majukumu ya wake hao.hatakua fataki kwa sababu wake watatu wanatosha. kuondosha kiu aliyokua nayo.unajua ukiwa na wake 3 ndio ushamba wa kumuona kila mwanamke mzuri unaisha kuoa wake watatu sio ujinga ndugu yangu acha jazba  mwanasheria wewe ndio tunakutegemea utetee haki za wanawake waolewe lakini unatetea wabaki mitaani kazi hawana  wakajiuze  aa mimi naona mweye busara na kama wewe ni mwanamke basi kubali ukewenza ingawa una changamoto zake   ahsanteni
Comment by neema molleli on February 1, 2011 at 1:20pm
mmmh wewe inaelekea unapenda wanawake sana,,,, sasa wazuri ndio hao wanazaliwa kila siku na wewe unaelekea uzeeeni,, si utakua fataki wewe jamani??
Comment by h.k.th on January 17, 2011 at 12:13pm

aah hongera bwana jitahidi na kulinganisha penzi lako lisiwe hafifu kwa mmoja

 

 

Comment by Mambo Jambo on January 14, 2011 at 5:00pm

Kweli ujinga umetawala ktk jamii za watu waishio dunia ya tatu,!! Adui mkubwa wa Tanzania ni Ujinga na Umasikini, Sasa mtu kama huyu alieshindwa kumiliki tamaa zake za kimalaya eti anasifiwa? 1)Ninahakika hana uwezo wa kuakamilishia mahitaji yao haswa elimu kwa watoto watakao zaliwa humo, 2) Watoto wanao zaliwa ktk family kama hii hua na mvutano chuki ambayo wakati mwingini husababisha kurogana na uana 3) Tasisi za kijamii nyingi zipo wapo wapi kuzungumzia tatizo kama hili ?? Wa Tanzania amkeni kupinga vitendo viovu ktk jamii yenu watoto wa mtaani hawata isha kwa mtindo huu.  

Comment by RAJAN HUSSEIN on January 13, 2011 at 9:44am
Congrats wa kitenge ila ningependa kushauri uwe mwenye jitihada za kuweka wakawa kitu kimoja kama wake zako na pia kushirikiana kwa kila hali.....basi utakuwa wa amani ktk ndoa zako kwani Fitna hazitokuwepo za kupitiliza...
Comment by Lucy Samwel on January 10, 2011 at 11:14am
Mmh! siyo sifa tena hata kama dini inaruhusu ndiyo ufanye hivyo
Comment by Mohamed Abdulaziz on September 19, 2010 at 8:23am
Safi sana Maulid, bado wawili mtu wangu! hadi nakuonea wivu mwana!
Comment by Joyce on July 12, 2010 at 8:53am
yaani we maulid ni mzuri ila unapenda sana wanawake acha hizo utakufa na ngoma
Comment by meggie impostra on July 11, 2010 at 7:40pm
hamna lolote tamaa zake na umalaya wake ndio wamfanya aoe kila kukichaaa ew mtt mdogo unakuwa na tabia kama za mababu zetu bwana ambazo siku hz wachache wanaozfuata kuoa wake wa 3 wa tano hata kama unawaudumia lkn kwa mtu kama wewe na ujana wako wala haipendezii kbsaaaa lol
Comment by Dinna on July 6, 2010 at 9:07am
Mh! hakuna cha udini wala nini kwa karne hii kijana mdogo kama wewe unaoa oa hovyo hata haipendezi kwani huyo mmoja umeshaweza kumtimizia haja zake? kwanza ni kumdhalilisha mkeo wa kwanza acha ushamba maulid unakuwa kama hujaenda hata darasa. Dini dini mbona viongozi wapo waislam na uwezo wao hawana zaidi ya mmoja acha kusingizieni dini ni tabia ya kutotulia na kupenda chini.

ADVERTISEMENT


Advertisement

 

Forum

KIPIGO CHA BAO 2-1 KWA MAN UTD, KOSA LA MWAMUZI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Mohammed Mar 26. 6 Replies

JE, NI KWELI KWAMBA KIPIGO CHA BAO 2-1 ILICHOKIPATA MAN UTD KUTOKA KWA REAL MADRID USIKU WA KUAMKIA LEO LAWAMA ZOTE ZIMWENDEE MWAMUZI WA MCHEZO AU MAN UTD WAJILAUMU WENYEWE? TUPE MAONI YAKO!!!

HALI INAYOENDELEA BUNGENI, SPIKA NA NAIBU WAKE WAMESHINDWA KUONGOZA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Ali Abdalla Ali Apr 22. 20 Replies

Tumeshuhudia kwa siku za hivi karibuni hali halisi iliyokuwa inatokea katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, kwa hali hii ni ishara kuwa Spika na Naibu wake washindwa kuliongoza bunge hilo?

VURUGU ZA CCM NA CHADEMA KUGOMBEA MLINGOTI WA BENDERA DODOMA, NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Phinehas Rishiansia Kileo May 3. 6 Replies

Wafuasi wa CCM wakimshambulia mfuasi wa Chadema mkoani Dodoma…

Tags: BENDERA, WA, DODOMA, NANI, KULAUMIWA?

VURUGU ZINAZOENDELEA HAPA NCHINI NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by NELSON UVAMBE yesterday. 27 Replies

HIVI KARIBUNI KUMEKUWEPO UPOTEVU WA AMANI HAPA NCHINI PAMOJA NA WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI. MKOANI KAGERA WANANCHI WENYE HASIRA WALIWAUA POLISI, IJUMAA ILIYOPITA WAKULIMA NA WAFUGAJI HUKO WILAYANI KILOSA WALIZUA VURUGU NA KUFUNGA BARABARA,…

MRISHO NGASSA KUPELEKWA SIMBA SC BILA RIDHAA YAKE, JE NI HALALI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Domino Bagambisa Jan 21. 17 Replies

Kiungo hatari wa Azam FC, Mrisho Ngassa leo amepelekwa Simba SC kwa mkopo na timu yake…

Tags: SOKA

hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Started by Gysper in Siasa. Last reply by Jamal amor May 9. 24 Replies

 hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Kauli Ya JK kuwa Mauaji ya Arusha ni "Bahati Mbaya"

Started by Kulikoni Ughaibuni in Siasa. Last reply by richardngeze Feb 12. 12 Replies

Tanzania tuna tatizo kubwa.Hakuna haja ya kunyoosheana vidole as to nani amechangia tatizo hilo bali cha muhimu na haraka ni namna tutakavyoweza kutatua tatizo hili.Nisimung'unye maneno: tatizo kubwa linaloikabili ni kuwa na Rais ambaye takriban…

Latest Activity

© 2013   Created by Global Publishers.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service