Na Richard Bukos
MAISHA ya msanii wa filamu Bongo, Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’ yako hatarini kufuatia ujumbe wa kumuua unaosambazwa na muongoza filamu, Mandela Nicholas ‘Jacob’ anayedai kudhulumiwa na msanii huyo kiasi cha shilingi 325,000.

Jacqueline Pentzel ‘Jack Chuz’.

Kwa mujibu wa ujumbe huo, jamaa huyo amedhamiria kumfanyizia Jack kwa kumcharanga mapanga kisa eti kadhulumiwa kiasi hicho cha fedha ambazo ni malipo ya kumuongozea filamu yake.
Jacob anadai kuwa, awali alimuandikia ‘script’ na kumuongozea filamu msanii huyo lakini kabla kazi haijaisha, wakazinguana hadi kufikishana katika Mahakama ya Mwanzo Ilala jijini Dar.
Hata hivyo, mahakama alimuamuru Jack alipe fedha hizo lakini kinyume chake msanii huyo akawa mgumu kutekeleza, hivyo kwa hasira Jacob akamuandikia Jack sms hiyo ya vitisho.
Sehemu ya ujumbe huo inasomeka hivi; “Labda kifo kiniite leo Jack nitamuua, kama laki 325,000 hajanipa mtasikia. Kama rafiki au ndugu jiandae na mazishi ya marehemu Jk Pentzel full panga tu.”
Sehemu nyingine ya ujumbe huyo ilisomeka hivi; “Wapendwa Jack anachohitaji sasa ni kifo na nitamuua kweli, mimi simsukumi…ila mapanga tu ndiyo dawa yake.
“Utapeli utamuua Jaki, leo kesho, keshokutwa mkisikia msiba ulizia kapigwa panga au? Kama siyo panga siyo Jacob, kama panga na vipande 150 ewaa. Yeye kaburini mimi Segerea. Jasho la mtu haliliwi.”
Akizungumza na mwandishi wetu kuhusiana na sms hiyo, Jack alisema kuwa naye ameipata na katika kujihakikishia usalama wa maisha yake amekwenda kuripoti polisi na kupewa RB.

Views: 2899

Tags: amani11

Comment

You need to be a member of Global Publishers to add comments!

Join Global Publishers

Comment by msichoke mlugu on December 24, 2012 at 9:57pm

unapewa rb hapo dawa kulipa tu ukimpa chake hana time na wewe mrembo unashindwa kulipo laki tatu aibu njoo nikukopeshe

Comment by mayalilwa on December 24, 2012 at 5:39pm

ni deni hilo tu au kuna visa vingine hamtaki kuvisema!

Comment by dinah kimz on December 22, 2012 at 9:31am

afeeeeeeeeeeeee

Comment by lumi mwandelile on December 19, 2012 at 12:48pm

ntakushukuruje, kwani hata mimi cmpendi huyo kidudumtu

Comment by richardngeze on December 15, 2012 at 4:51pm

Duh! mapanga "shaaaa"! haya bwana nawatakieni safari njema huko mtakapoenda baada ya kitendo.

Comment by mnasa mohd on December 15, 2012 at 2:18pm

jacob maneno ulio sema simazuri  huyu dada akiuwawa na mtutu yoyote basi juwa kama weye ndio utakamatwa ju umeisha tangaza kuuwa ila mimi na waza huna akili hata sura yako inaonesha kama unakitu tafauti na binaadamu wangine je wewe unajiona uko sawa ????

Comment by uncle sam on December 10, 2012 at 10:06pm

mdomo huo uliponza kichwa jacob

Comment by FURAHA TAUSI on December 10, 2012 at 4:21pm

WEE JACOB NAONA UNA UCHIZI ..NA WEWE JACK LIPA DENI LA WATU MBONA NI HELA NDOGO SANA KWAKO HIYO? TAFUTA PEDESHEE MMOJA AKULIPIE

Comment by Domino Bagambisa on December 7, 2012 at 1:19pm

jack lipa hiyo pesa na Jacob kwa nini unakosa busara mpaka umtishie mtu kifo ndo akulipe? Unakatisha tamaa.

Comment by mammy on December 7, 2012 at 12:23pm

sasa si ulipe?

ADVERTISEMENT


Advertisement

 

Forum

KIPIGO CHA BAO 2-1 KWA MAN UTD, KOSA LA MWAMUZI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Mohammed Mar 26. 6 Replies

JE, NI KWELI KWAMBA KIPIGO CHA BAO 2-1 ILICHOKIPATA MAN UTD KUTOKA KWA REAL MADRID USIKU WA KUAMKIA LEO LAWAMA ZOTE ZIMWENDEE MWAMUZI WA MCHEZO AU MAN UTD WAJILAUMU WENYEWE? TUPE MAONI YAKO!!!

HALI INAYOENDELEA BUNGENI, SPIKA NA NAIBU WAKE WAMESHINDWA KUONGOZA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Ali Abdalla Ali Apr 22. 20 Replies

Tumeshuhudia kwa siku za hivi karibuni hali halisi iliyokuwa inatokea katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, kwa hali hii ni ishara kuwa Spika na Naibu wake washindwa kuliongoza bunge hilo?

VURUGU ZA CCM NA CHADEMA KUGOMBEA MLINGOTI WA BENDERA DODOMA, NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Phinehas Rishiansia Kileo May 3. 6 Replies

Wafuasi wa CCM wakimshambulia mfuasi wa Chadema mkoani Dodoma…

Tags: BENDERA, WA, DODOMA, NANI, KULAUMIWA?

VURUGU ZINAZOENDELEA HAPA NCHINI NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by NELSON UVAMBE on Monday. 27 Replies

HIVI KARIBUNI KUMEKUWEPO UPOTEVU WA AMANI HAPA NCHINI PAMOJA NA WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI. MKOANI KAGERA WANANCHI WENYE HASIRA WALIWAUA POLISI, IJUMAA ILIYOPITA WAKULIMA NA WAFUGAJI HUKO WILAYANI KILOSA WALIZUA VURUGU NA KUFUNGA BARABARA,…

MRISHO NGASSA KUPELEKWA SIMBA SC BILA RIDHAA YAKE, JE NI HALALI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Domino Bagambisa Jan 21. 17 Replies

Kiungo hatari wa Azam FC, Mrisho Ngassa leo amepelekwa Simba SC kwa mkopo na timu yake…

Tags: SOKA

hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Started by Gysper in Siasa. Last reply by Jamal amor May 9. 24 Replies

 hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Kauli Ya JK kuwa Mauaji ya Arusha ni "Bahati Mbaya"

Started by Kulikoni Ughaibuni in Siasa. Last reply by richardngeze Feb 12. 12 Replies

Tanzania tuna tatizo kubwa.Hakuna haja ya kunyoosheana vidole as to nani amechangia tatizo hilo bali cha muhimu na haraka ni namna tutakavyoweza kutatua tatizo hili.Nisimung'unye maneno: tatizo kubwa linaloikabili ni kuwa na Rais ambaye takriban…

© 2013   Created by Global Publishers.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service