Kazi afanye mume, mshahara kupewa mke

Mshahara sasa kwenda kwa mke

Maafisa katika jimbo la Gorontalo nchini Indonesia wamepata njia mpya ya kuhakikisha wake wa wafanyakazi wa serikali wanapata mgao wa kutosha wa mshahara wa waume zao.

Mpango huo ni kuweka fedha za mishahara katika akaunti za benki za wake wa wafanyakazi wa serikali. Mpango huo unatazamiwa kuanza mwezi Machi na unatarajiwa kuweka familia pamoja, kutokana na kongezeka kwa vitendo vya wanaume kutumia fedha za ziada kwa wanawake wa nje.

Ni mpango rahisi lakini wa aina yake. Kuanzia mwezi Machi, kila mwanaume aliye na mke na anayefanya kazi katika serikali katika jimbo la Gorontalo atashuhudia mshahara wake ukiingia kwanza katika akaunti yake na mara moja fedha hizo kuhamishwa kwenye akaunti ya mke wake.

Hatua hiyo ni ya kuzuia matumizi "mabaya" ya fedha. Maafisa wanasema wamepokea malalamiko mengi mwezi uliopita kutoka kwa wake wa wafanyakazi wa serikali, ambao wanasema hwapati fedha za kutosha kutoka kwa waume zao kwa ajili ya matumizi ya nyumbani.

Msemaji wa jimbo la Gorontalo Rudy Iriawan amesema kanuni hiyo mpya ina lengo la kulinda familia zisimeguke. "Tuna wasiwasi kwa kuwa mwanaume ndio anadhibiti fedha za familia.

Na tunataka kuhakikisha mishahara ya wafanyakazi wa serikali inatumika kujenga familia na sio kwa ajili ya mambo mengine hasa wanawake wa nje".

Hata hivyo maafisa hao pia wameonya kuwa wake wa wafanyakazi hao wa serikali wasitumie fedha kujinunulia vitu vya kifahari.

Wametakiwa kuzingatia hatua hiyo kama kazi, zimesema mamlaka, katika kutazama fedha za familia za nyumba zao.

chanzo na bbcswahili

Views: 522

Tags: Kazi, afanye, kupewa, mke, mshahara, mume

Comment

You need to be a member of Global Publishers to add comments!

Join Global Publishers

Comment by Babu Lao on February 14, 2012 at 1:37pm

SAFI SANA, VERY NICE IDEA!!!

Comment by samora rajab albert on February 11, 2012 at 7:19pm

ikifika TZ iyo am sure wanawake watazidi kukoma, mana ukishapata mgao tu mume hakujui tana itoshe isitoshe utajijua mwenywewe

Comment by Mawazo Katota on February 11, 2012 at 12:20am

Kwa jinsi tunavyopenda kuiga sasa hivi tutaanza kusikia kelele za wanaharakati wa haki za mwanamke. Wakianzisha hilo nitakuwa mvuvi na samaki nitauzia baharini

Comment by MARIA ROSSA on February 10, 2012 at 9:19pm

Ikija bongo ndoa zitavunjika balaa, wanawake full kujiachia Dar live na watoto hata socks za shule hawatapata, kitchen part na michiriku kila leo. Kila mtu ashike kile anachokichuma na asiyeweza kuhudumia watoto akafie mbali na Mungu amlaani.

Comment by Isalia on February 10, 2012 at 6:16pm
Ikija bongo naacha kazi ya serekali siwezi kusumbuliwa kwa pesa yangu
Comment by kibabaa on February 10, 2012 at 5:41pm

Huu ndio mwisho wa watu kuoa, zinaa itakomaa, je mume akisema kuwa hakuweza kuja kazini kwakuwa hana nauli nani awajibike. mimi sikudhani watu wa karne hii wanaweza kuwa na mawazo ya kipumbavu kama hayo. ina maana kuzaliwa mwanamke ndio ufunguo wa kuwa tajiri, ndio maana ndo za jinsi moja zinapamba moto, mwisho wa dunia, walioshangilia hapa utakuta hawaelewi madhara yake. je na wanawake waofanya kazi mishahara yao iende wapi?

Comment by Suleiman Abdalla Salim. on February 10, 2012 at 4:53pm

Hili kidogo lina utata!

Comment by julius manning on February 10, 2012 at 4:49pm

ha ha ha hao hawajafanya lolote zaidi ya kuwapelekea wanawake wabadilishe Serengeti boys kila kukicha.

Comment by marimar ethan on February 10, 2012 at 3:26pm

HEHEHEEEEEE kumbe hata uko yapo yanii gud job nimeipend sn aisee hata uku wafanyiwe hivyo hvyo maana wanawk tunapata tabu uwiiiiiii

Comment by kaka on February 10, 2012 at 2:30pm

NA BONGO LETA TUMALIZE VIBANDA VYA NYUMA NIPO NAWE DADA LUMI MWANDELILE NA BONGO TUFANYE KAMA WAO


ADVERTISEMENT


TANGAZA HAPA

ADVERTISEMENTS

Latest Activity

GUNZ TRUVADA posted a status
"KUMPA ASIYE KUPA NI SAWA SAWA NA KUTUPA"
4 minutes ago
GUNZ TRUVADA posted a status
"KUMPA ASIYE KUPA NI SAWA SAWA NA KUTUPA"
5 minutes ago
othman Ochu posted a status
"SCENE 1 WAHUSIKA: AMIDU , SHARIFA MAHALI: ZANZIBAR MUDA : JIONI ( WAKIWA WANASHUKA TOKA KATKA BOTI YA JION KUINGIA KATKA MJI WA ZANZI"
9 hours ago
Priscus Adelard shared GLOBAL's blog post on Facebook
9 hours ago
mrembo commented on julius manning's photo
Thumbnail

Mtanzania huru

"pole sana usijali iko siku mungu atakujaalia mungu hamtupi mja wake"
10 hours ago
mrembo commented on Sili Silali's photo
Thumbnail

Duh!

"mama mzima hayawani mavazi gani hayo takupa mfano chungwa likiwa halijamenywa unatamani ulile…"
10 hours ago
kaka commented on Ali Amur Ali's video
Thumbnail

AZIMIO LA KUANGAMIZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE

"hapo ni kina dada kutua comment zao"
10 hours ago
Gaston Kayombo commented on Ali Amur Ali's video
12 hours ago
roylicious and Jackson Jacob are now friends
12 hours ago
babu wa loliondo (cup) updated their profile
12 hours ago
julius manning commented on julius manning's photo
Thumbnail

vijana 2016 itakuwa hivi

"@furaha mimi ni kikongwe hayo ni kazi kwako."
13 hours ago
Masalu Mayeji Many'hasimha shared GLOBAL's blog post on Facebook
13 hours ago

© 2012  

Designed & Developed by
G5 CLICK COMPANY.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service

How to make a Website