ARTHUR akiwa mikononi mwa mzee Mwandambo, alijilaumu sana moyoni mwake, alijiona mpumbavu sana kuamua kurudi Dar badala ya kuendelea kujificha Lindi. Aliamini alishakifikia kifo chake.
Tofauti na matarajio yake, baada ya mzee Mwandambo kuondoka naye, alimuuliza mambo mengi kuhusu historia ya maisha yake, alipogundua kwamba alikuwa yatima, akaamua kumsaidia fedha.
Arthur bila kutegemea kabisa, alisalimika mkononi mwa mzee Mwandambo, akashuka garini akiwa na fedha zake kisha akatafuta usafiri mwingine. Safari ya kuelekea Chanika ikaendelea.
Mzee Mwandambo alikuwa na wasiwasi mwingi sana, alishangazwa na jinsi mwanaye Nicole alivyoonekana kukosa furaha baada ya Arthur kukamatwa. Alihisi kuna kitu kinaendelea ndiyo maana alipoteza furaha ghafla.
Alipomwuliza Nicole, hakuonekana kuwa na jibu lolote, zaidi ya kuonekana kuwa na kigugumuzi kikali huku macho yakiwa yamemkodolea baba yake.
Je, nini kitatokea? SONGA NAYO...
Mimi ni baba yako, tena unatakiwa kufahamu kwamba, nimetangulia kuiona dunia. Hebu niambie ni nini kinaendelea?” mzee Mwandambo akakazia msimamo wa swali lake huku akimwangalia mwanaye usoni.
Nicole alitakiwa kuwa makini sana, jibu la swali aliloulizwa lingeweza kuwa dawa au tatizo zaidi kwa baba yake. Ubongo wake ukafanya kazi kuliko kawaida, akajipa matumaini. Akapiga moyo konde na ghafla akavaa ujasiri.
“Baba sijakuelewa vizuri unachomaanisha.”
“Hivi ina maana hujanisikia au?”
“Baba unazungumzia kuhusu ajali?”
“Ndiyo.”
“Hata wewe naamini ulichanganyikiwa, ndiyo maana ulishuka kwa hasira na kumchukua yule kijana. Kama ilivyo kwako, kwangu pia ilikuwa hivyo hivyo. Sikuwa na amani baada ya kukaribia kumgonga yule kijana.
“Kwa kiasi kikubwa sana nilihisi ulikuwa unataka kumdhuru, ndiyo maana nikapatwa na simanzi ya ghafla moyoni mwangu na kuwa na wasiwasi mwingi, maana nilihisi kwamba ungeweza kumdhuru.”
“Hilo tu!”
“Ndiyo baba.”
“Si kweli.”
“Kama si kweli, sasa ukweli ni upi?”
Mzee Mwandambo alikaa kimya kwa muda, kilipita kimya cha zaidi ya dakika tatu, alipoanza kuzungumza baadaye alikuwa anaongelea kitu kingine kabisa.
“Lakini mwanangu, unaionaje hii shule?”
“Nzuri sana baba. Naona ni nzuri na inavutia sana.”
“Sasa kama ndivyo una sababu gani ya kuhangaika na wapuuzi wasio na maana?”
“Kwa kweli baba sina. Nimeona wazi makosa yangu.”
“Kuona makosa si tija Nicole.”
“...pia nimekubali kubadilika baba. Ni ahadi ambayo hata mama anaijua.”
“Nitafurahi sana ikiwa hivyo mwanangu.”
“Imeshakuwa baba, siwezi kuidhulumu nafsi yangu.”
“Vema. Naona turudi nyumbani sasa.”
“Sawa baba!”
“Vipi kuhusu mtoko wa kesho? Natamani sana niende nanyi mahali.”
“Ni wazo zuri baba.”
“Unapenda wapi?”
“Unanijua vizuri sana baba, ufukweni ni sehemu ambayo moyo wangu huridhika zaidi nikienda.”
“Sawa.”
Hawakukaa sana, walizungumza machache na mafundi, kisha wakaingia kwenye gari na kurejea nyumbani kwao, kisiwani Bongoyo.
***
Mpaka muda huo akiwa amesimama mapokezi, Arthur alikuwa hajaamini kama ni kweli alipona katika mkono wa mzee Mwandambo. Alihisi alipata bahati ya kipekee, maana kwa kiasi kikubwa alitarajia kuingia mikononi mwake.
Alijiandikisha kwenye Gesti hiyo, iliyokuwa ndani ndani kabisa, eneo la Manzese Tip Top. Alitamani sana kumpigia Nicole lakini alishindwa, maana walikubaliana kwamba hatakiwi kumpigia simu mpaka Nicole mwenyewe atakapoamua kufanya hivyo.
Aliingia ndani ya chumba chake na kuanza kutafakari tukio zima lilivyokuwa, akashindwa kuelewa kabisa, kitu pekee alichokifanya kwa wakati ule ilikuwa ni kumshukuru Mungu.
***
Zoezi la kumsaka Arthur mjini Lindi lilifanyika kwa kasi na kwa kutumia mbinu zote bila mafanikio. Ni kama Lindi ilifunikwa na kufunuliwa, lakini Arthur hakupatikana.
Baada ya wiki mbili, Tino na wenzake walirudi kwa mzee Mwandambo na kumweleza namna walivyohangaika lakini bila mafanikio yoyote.
“Umemtafuta vizuri Tino?”
“Sana Chief, kitu ninachotaka kukuambia ni kwamba, Arthur hayupo Lindi, kama angekuwepo lazima tungemtia mkononi.”
“Sawa, achaneni naye kabisa. Hili jalada nimelifunga rasmi.”
“Sawa Chief.”
Tangu hapo mzee Mwandambo aliamua kuacha kumfuatilia Arthur kwa uwazi, lakini kichwani mwake alipanga kumsaka kimya kimya. Ndicho kitu kilichokuwa kichwani mwake.
***
BAADA YA MIAKA MITATU
Arthur aliendelea kuishi katika Gesti ile kwa siri, msaada mkubwa akiwa anaupata kwa Nicole. Aliendelea kuwasiliana na Nicole kwa siri kubwa na mara kadhaa walikuwa wakikutana na kufanya mapenzi bila kugundulika.
Tayari Nicole alikuwa ameshafika kidato cha pili, muhula wa mwisho akikaribia kabisa kuanza kidato cha tatu. Pamoja na umri wake mdogo, alionekana msichana mkamilifu. Alikuwa na kila kitu kinachopaswa kuwa na mwanamke ambaye tayari ana mtoto!
Nicole alibadilika, alikuwa msichana anayejipenda, mwenye maringo na anayejua thamani yake kama msichana. Hata Arthur naye alikuwa na mabadiliko makubwa sana, alikuwa kijana anayevutia sana.
Alivaa vizuri na kula mlo safi, afya yake ikaimarika, pamoja na kwamba alikuwa akiishi katika hofu kuu. Akiwa katika Gesti hiyo anayoishi, alikutana na kijana mmoja aliyeitwa Emmanuel.
Emmanuel alionekana kuvutiwa sana na Arthur. Alikuwa mfanyabishara anayefanya shughuli zake katika nchi za China na Ujerumani. Alifika nchini Tanzania kwa shughuli zake za kibiashara.
Alitamani sana kushirikiana na Arthur. Akaamua kumweleza ukweli.
“Tangu nimekuona hapa, nakuona una kitu cha tofauti kabisa ambacho kama ukisaidiwa unaweza kubadili maisha yako,” Emmanuel akamwambia Arthur.
Arthur akashtuka. Hakutegemea kusikia maneno hayo kutoka kwa mfanyabiashara mkubwa kama Emmanuel. Akakaa sawa akimsikiliza kwa makini.
Je, nini kitaendelea? Usikose kufuatilia katika Gazeti la Championi Ijumaa.
Comment
Comment by vincent on March 2, 2012 at 2:11pm haaaahhaaaa kama mimi vile miaka mitatu kwa siri kuu
Comment by Real De' Dear on February 27, 2012 at 1:50pm wanasema ridhiki ya mbwa iko miguuni.
Comment by hamisi mohamed juma on February 24, 2012 at 5:43pm
Comment by Jamaldin A Issa on February 24, 2012 at 4:36pm
Comment by Emmanuel Mallewo on February 24, 2012 at 12:35am EMMANUEL atampeleka Arthur nje atakuwa mfanya Biashara mkubwa na atakuja kumwoa Nikole kirahisi
Comment by DORAH FREDY on February 23, 2012 at 2:02pm
Comment by rosetarimo86 on February 23, 2012 at 11:35am bg hap shigongo
Comment by Kidugwa Ramadhani on February 23, 2012 at 6:38am
Comment by dorice damian nkane on February 23, 2012 at 12:14am Hofu yangu ni kwa aina na biashara, we emma usimwaribu mkwe wa mwandambo huyo.
Inafurahisha
| 1 |
GLOBAL |
| 2 |
julius manning |
| 3 |
Man KKK |
| 4 |
Sili Silali |
| 5 |
IL-YA |
| 6 |
chama baby |
| 7 |
msichoke mlugu |
| 8 |
kaka |
| 9 |
Maji Marefu |
| 10 |
Kelvin Luhala Eto'o |
othman Ochu posted a status
mrembo commented on Sili Silali's photo

You need to be a member of Global Publishers to add comments!
Join Global Publishers