GLOBAL

HASHEEM KUMBONDA TID, FULL MUVI!

Na Mwandishi Wetu
Bado Jiji la Dar limegubikwa na tukio la nyota wa Ligi ya NBA nchini Marekani, Hasheem Thabeet Manka kumkata mtama wa ‘kushiba’ msanii nyota wa Bongo Flava, Khaleed Mohamed ‘TID’, Amani limegundua.
Mbaya zaidi, hali hiyo inakwenda sanjari na utata wa nini hasa kilisababisha tafrani ya nyota hao ambao wanafahamiana vizuri. Gazeti hii lilikwenda mbele zaidi na kusaka ukweli wa pande zote na ifuatayo ndiyo full muvi.

KWA MUJIBU WA SHUHUDA
Anasema ilikuwa mishale ya saa kumi usiku, Ijumaa ya Mei 7, 2010 ndani ya Club Billicanas ambapo msanii wa Bongo Flava, TID aliingia akiwa ameambatana na kimwana.
Akazidi kuweka wazi kuwa, TID na demu huyo walionekana kuzunguka zunguka na kusalimiana na baadhi ya watu lakini muda si mrefu, aliingia Hasheem akiwa ndani ya gari lake la kifahari aina ya Range Rover Sport jeusi lenye namba za usajili T SSS 101.

Hasheem Thabeet
Shuhuda huyo anasema kuwa, nyota huyo akiwa na wapambe wake wawili alikwenda kukaa kaunta na kuanza kuagizia vinywaji, lakini ghafla TID akiwa na kimwana wake walipita jirani na Hasheem, “yule demu akamwita Hasheem, kisha akaenda kumsalimia, lakini TID akaenda mbele na kusimama akiwaangalia,” alisema shuhuda huyo.
Akizidi kuweka wazi tafrani nzima, sosi huyo anasema: “Ghafla TID alisema umemwona huyo tu (yule demu), sisi wengine hukutuona.”

Anaendelea kusema kuwa, Hasheem akiwa amevalia ile kapero yake alimjibu TID kuwa, hakumwona lakini si mbaya akamsalimia mambo vipi?
Shuhuda huyo makini anasema kuwa, TID huenda alikuwa na lake jambo kwani pamoja na salamu hiyo alianza kumtukana jamaa (Hasheem) huku akimwambia maneno ya kejeli, “lakini jamaa alikuwa akimuonya kuacha kumtukana,” alisema.

Akasema baadhi ya watu waliokuwemo ndani walianza kuhisi kitu kwani walisikika wakisema TID anataka kufanya vurugu kutokana na historia yake anapokuwa Club au sehemu mbalimbali za burudani.
Shuhuda huyo anaendelea kusema: “Ukweli Hasheem alimwonya TID karibu mara nne aache kumsemea mbovu, lakini jamaa akaendelea hadi Hasheem akashikwa na hasira na kusimama, TID akasogea mbele lakini huku akiendelea kumtukana jamaa.”

Khaleed Mohamed ‘TID’
Anasema TID alipomwona Hasheem anazidi kumfuata, akakimbilia nje ndipo Hasheem alipomkimbiza hadi huko na kumpiga mtama huku akimuuliza ni kwanini amemtukana bila sababu licha ya kumwonya kuacha kufanya vile.
Sosi anamwaga zaidi kwa kusema kuwa, baadhi ya watu ndani ya ukumbi walisikika wakisema kwa hatua aliyofikia TID, hata angekuwa nani asingeweza kuvumilia maana alimtukana karibia mara kumi.
Akasema: “Tena ana bahati sana, Hasheem kampa nafasi mara nne akimwonya asiendelee kumtusi, lakini hakusikia.”

Inadaiwa zaidi kuwa, wapambe na mabaunsa walimfuata Hasheem na kumvutia pembeni ndipo nyota huyo ambaye yupo Bongo kwa mapumziko, akaamua kuondoka zake akimwacha TID akiugulia maumivu chini.

ANAVYODAI TID MWENYEWE
Baada ya kimbembe hicho, msanii huyo wa Bongo Flava aliamua ‘kumwaga mboga’ akisema kile kilichojiri hadi kujikuta akilimwa mtama na nyota mwenzake huyo.
Anasema: “Ilikuwa saa kumi na nusu nikiwa natoka Club Billcanas na rafiki yangu Anna huku naongea na simu na Hisbert (sijui ni nani?) kwa sauti ya juu maana kelele za muziki zilikuwa zinasumbua, nikiwa nimesimama nje ya mlango wa kioo ghafla akatokea Hasheem ambaye alikuwa ‘Kaunta’ akiongea na wakata tiketi, akanipiga bonge la mtama nikaanguka chini na kuzirai kwa dakika kadhaa.

“Mabaunsa wakanibeba na kuniweka pembeni maana nilikuwa mlangoni, nilipozinduka nilisikia maumivu makali kwenye mabega, mkono wangu wa kulia na mguu ambao unafanya kutembea kwangu kwa taabu, nikaangalia mkononi simu yangu sikuiona, nikawauliza mabaunsa yule jamaa amekwenda wapi, wakadai ameondoka tayari…

“Nikajikokota kuelekea kwenye gari yangu na kuelekea Polisi kutoa taarifa niweze kupata matibabu. Nilipofika nikaandika statement na kupewa namba ya case CD/RB/6848/10 pia nikapatiwa PF3 (Fomu ya Polisi namba 3) nikaenda hospitali kupata matibabu.
“Sasa hivi (Jumanne) niko kitandani siwezi kutembea vizuri, pia nitashindwa kuperfom (kutumbuiza) kwenye harusi ambayo tayari nimeshalipwa pesa.”

SWALI LA TID
“Swali langu ni kwanini ameamua kunidhalilisha vile mbele ya CLUB na FANZ (mashabiki) ambao nilikuwa nawatumbuiza? Kwanini ameamua kuniharibia kazi yangu? Kwanini ameamua kunipiga bila ya kumkosea? Je, ni sawa hivi jamani….naona machozi yananitoka sina cha kumweleza mama yangu.”

ALICHOSEMA HASHEEM
Baada ya maelezo hayo, Amani liliongea na Hasheem Thabeet ambaye kama TID ‘alimwaga mboga’, yeye ‘amemwaga ugali’ ambapo anadai TID ni mchokozi.
Anasema kuwa, siku ya tukio akiwa na kampani yake walikwenda Club Billicanas, wakaingia ndani ‘kujiachia’.
Hasheem anasema: “Tulikwenda kukaa Kaunta na kwa sababu huwa nakunywa kwa kusaini mahali, nilifanya hivyo, mhudumu alinipa kalamu na kitabu cha kusaini.”

Anasema akiwa anamwaga wino, alisikia sauti ya kike ikimwita kwa jina, Hasheem! Akaacha ‘kuanguka kitabuni’ na kuangalia ilikotokea sauti hiyo.
Anasema: “Nilimwona msichana mmoja akiwa ameongozana na TID. Lakini yule msichana alikuja nilipo, akajitambulisha, nikawa najaribu kumkumbuka. Wakati huo TID alikwenda hatua kadhaa mbele na kusimama akituangalia.
“Ghafla akasema nimeona wengine tu, yeye (TID) sikumwona. Nikamjibu ni kweli sikumwona, ila yeye kwa sababu ndiye aliyeingia, alipaswa kunisalimia iwapo aliniona kama alivyofanya yule msichana aliyeongozana naye,” alisema Hasheem.

Akasema, lakini majibu ya Mbongo Flava huyo aliyewahi kufungwa jela kwa kosa la kumpiga mtu, hakuyategemea, kwani alimwambia asijifanye yeye (Hasheem) ni staa sana, hana lolote.
Hasheem anasema alicheka akiamini TID alikuwa akimtania tu, lakini akakasirishwa na staa huyo kumwambia ‘unacheka nini sasa’.
“Niliamua kucheka kwani TID namfahamu siku nyingi, lakini aliponiambia unacheka nini sasa, ndipo nikajua kumbe yupo kishari, nikamwonya kuwa, asiendelee kunisemea mbovu.”

Anasema licha ya kumwonya mara ya kwanza, ya pili na ya tatu, TID aliendelea kusema ‘mbofumbofu’ hali iliyompandisha hasira nyota huyo na kuamua kutoka naye ‘baruti’ mpaka nje ambako alipom’bamba alimpa mtama wa sawasawa, jamaa akaenda ‘dauni’.
Anasema alipoona jamaa hasimami kujibu mapigo, yeye aliamua kutimua zake ‘mahom’ Sinza lakini baadaye alifuatilia na kuambiwa msanii huyo aliamka na kuondoka zake.

SWALI LA HASHEEM
“Ni kwanini TID aliamua kunisemea mbovu huku nikimwonya mara tatu asiendelee kufanya vile? Je, alitaka litokee lililotokea ili tuhadhiriane mbele za watu? Nimesikitika sana, mimi sina historia ya kudundana na watu katika maisha yangu.”
Wakati huo huo, habari zinadai kuwa, mmiliki wa Billicanas, Freeman Mbowe amempiga marufuku TID kuingia kwenye ‘kiwanja’ hicho baada ya kuzidi kuendeleza tafrani usiku huo huku yeye mwenyewe Mbowe akishuhudia.

Views: 199

Tags: amani11

Comment

You need to be a member of Global Publishers to add comments!

Join Global Publishers

Juma Bahati Comment by Juma Bahati on May 22, 2010 at 7:08pm
Usikute walishakula na kijambio chenyewe na sasa kanogewa anataka kurudi tena.
BARAKA NSWILA Comment by BARAKA NSWILA on May 17, 2010 at 3:59pm
mbowe kafanya la msingi maana hao mastaa wa kibongo wamezidi kuuletea ulimwengu wa mastaa aibu
Claire Anthony Comment by Claire Anthony on May 15, 2010 at 5:19pm
Huyo TID ana matatizo siku nyingi tu sasa inabidi watu wamchukulie kama alivyo ,kwani ni difficult person,nilichoshangaa ni kwamba Hashim anamuelewa matatizo yake huyo jamaa kama angeamua kuuchuna angeonekana ana akili lakini amemkimbiza na kumpiga mtama wote wameonekana machizi ,jamaa hata huko USA bado hakujambadilisha naye.By Ally Moda
chapombe Comment by chapombe on May 14, 2010 at 11:05pm
halafu tid ukiingia kwenye anga za watu inaonekana watakuumiza,manaake naona hizo comments humu inaelekea wanahasira na wewe.na hii yote ni kwasababu unapenda vurugu bila mpango kila mara.wewe walivyokupeleka jela watu walikusikitikia sana,mimi nilifikiri ilikuwa fundisho kwako na mabongo fleva wenzio,kumbe hovyoo.kule ngome ilitakiwa wakora wangekula kijambio ndo ungetulia.
lilian ernest bitegeko Comment by lilian ernest bitegeko on May 14, 2010 at 9:28am
TID kazidi jamani anboa kila sehemu anyoeenda antk tujue kafika kwa kupitia ugomvi ama makelele kumsalimia mtu si hoja ye angegombana na demu wake na si hasheem tn kaonywa yani hata ingekuwa mimi ningemlza mabuti ingawa ni demu kwa kuwa wakti anamdhalilisha yeye alikuwa haoni ila alivyopigwa ndi akajua anadhalilishwa he neva gona change kweli hata haya demu wake nampa sory.TID NEVER CHANGE na itamharibia soko akiendelea hivyo
Honest K. Baitani Comment by Honest K. Baitani on May 14, 2010 at 4:32am
Hello Mzee Mwenda nakuaminia kwa point..!! .Dennis umesema kitu cha kweli lakini unafikiri ni vizuri sana angemuacha wamalizane baadae, baada ya T.I.D kumalizana na chuda wake, ila unafikiri ni rahisi hivyo. Hapa kila mtu alitaka kujionyesha kwa dem kuwa yeye ni zaidi, ila ingekuwa jambo la bsara anayekunywa kwa "signature" adahrau tu hii issuue hasa kwa aijili ya usalama wa kibarua chake, maana hapo tayari ameishafua back ground yake kwa domestict/social violence, this can be a felon, and may cost hima lot, and he might come to reget in here.
denis victor Comment by denis victor on May 13, 2010 at 7:11pm
TID yuko vizuri hata hashim namkubali saana bt ishu izo za kishamba since mchiz yuko na chuda angemchunia tu wabonge baadae.af uyo mrembo kakosea angeenda na tid mpaka kwa hashim then watambulishane!!!ila tid askonde madem wa bongo ndo walivyo!!!!hawakupaswa kufika huko kisa demu af tid temana na uyo manzi then mmalizane na mchiz kisela!!!akileta zipi mwache achape lapa kkiukweli woote hamna lolote kama mimi tu!!!
Anselm Comment by Anselm on May 13, 2010 at 6:07pm
Mimi wote wa'3(Hasheem,TID na huyo Kicheche aliyekuwa naye wana makosa):-
Hicho Kicheche kilishoboka na hizo ndo za mademu wa kibongo whether wanakubali or not,TID naye alileta ushamba na kinachomsumbua huyo ni Uswahili,kuzaliwa sijui kukulia uswahilini Kinondoni madongo kuporomoka kumemuathiri sana,kubadirika huyo ni ngumu sijui hata asaidiwaje
Sasa huyo Super wa Ma'superstar na yeye kaniacha hoi sana,hv yeye ni wa kukimbizana na Chokoraa TID kweli,eti hadi nje ya ukumbi na kumkata mtama...this is funny jamani,kwanini asingemkabidhi kwa wapambe wake,nini sasa faida ya kutembea na wapambe? hivi angemkuta TID ni Chuma cha pua akamtoa manundu ingekuwaje?
Aache ujinga,hivi uongozi wa Memphis wakisikia kuwa anapigana uswahilini unafikiri watamuacha hivihivi,huyu Jamaa mimi nafikiri na yeye si mzima,kwanza anatakiwa arudi kibaruani kwake ashauza sura sana ksbb naona uko anapoelekea atakuja kuharibu mazima.
Anselm Comment by Anselm on May 13, 2010 at 5:47pm
Wapi "Aha" naona agenda ya Bwana..ooh sorry Rafiki yake iko hewani.
ally mohammed ummiy Comment by ally mohammed ummiy on May 13, 2010 at 4:57pm
hiyo ishu ipo complicayed kidogo ila hashim alitakiwa kutake easily coz nn maana ya xposure? thn TID amn't sure km ilivyotokea ndivyo unavyoelezea ila kiakili haingii s kwamba namdiss noooooo.......ila for sure namfaham TID by da way tunatakiwa kujiepusha na skendo zisizo za lazima

ADVERTISEMENT

TANGAZA HAPA

ADVERTISEMENTS

Latest Activity

Profile Icon
Profile Icon
ALEIN ERICK OMARI commented on Dongonyo Juniour's photo
akili zake hazijatimia huyo  
1 hour ago
Profile Icon
kumekucha na makucha yakee!
Status posted by haji shehe (ustadh 2 hours ago
Profile Icon
Matilanga Lukingita commented on kadama J'z's photo
Kadama nipe namba yake mi nikafanye utafiti na kuwaondoa mashaka wadau. Uuuuwiiiiii !! hii kitu si…
3 hours ago
Profile Icon
kadama J'z commented on kadama J'z's photo
@ babjoga kila siku wana yaona kwenye TV kwanini wasi yajue
3 hours ago
Profile Icon
sammy updated their profile 3 hours ago
Profile Icon
kadama J'z commented on kadama J'z's photo
hahaa @ gervas angalia hayafai haya shauri zako @ babjoga angalia usije ukalia wewe @ miwani hilo…
3 hours ago
Profile Icon
kadama J'z commented on kadama J'z's photo
hahaa@ lumi, abbygirl,furaha & hadija acheni woga bana hao hatawakiingia ndani hawana issue…
3 hours ago
Profile Icon
Martha Jacob MJ's liked GLOBAL's blog post 'WEMA: DIAMOND ANA NUKSI' 4 hours ago
Profile Icon
bwire raphael updated their profile 5 hours ago
Profile Icon
13 blog posts by GLOBAL were featured 5 hours ago
Profile Icon
Mawazo Katota commented on GLOBAL's blog post 'Kivazi cha nusu utupu chamtia aibu Mona ukumbini'
Kaona ana miss headlines za udaku ameamua bora kulazimisha kidizaini. Hana haya wala hajui vibaya.…
5 hours ago

© 2012  

Designed & Developed by
G5 CLICK COMPANY.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service