Wagonjwa wote wa kisukari waliokunywa dawa kwa Mchungaji Ambilikile Masapile ‘Babu’ kijijini Samunge, Loliondo watakufa (au watapukutika) ikiwa wataacha kutumia dawa za hospitalini, Uwazi limegundua.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa gazeti hili, watu wengi waliokunywa dawa ya Babu ambao walikuwa na ugonjwa wa kisukari wamefariki dunia baada ya kuacha kutumia dawa za hospitalini.
Baadhi ya ndugu waliozungumza na gazeti hili walisema kuwa, mara baada ya ndugu zao kunywa dawa ya Babu, waliacha kunywa dawa za hospitali na matokeo yake sukari ilipanda au kushuka, hivyo wakaaga dunia.
Ndugu wa marehemu Juliani Lyasenga mkazi wa Arusha ambaye alibahatika kunywa dawa ya Babu kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kisukari, alikufa baada ya kuacha kutumia dawa kama alivyoelekezwa na daktari wake.
Mwingine ambaye alikufa baada ya kunywa dawa ya Babu kutokana na kuugua kisukari ni John Piswa, mkazi wa Tandika, Rafael Kisijo mkazi wa Kijitonyama, Saidi Mohamed mkazi wa Buguruni na Hausi X. Hollo “HH”, mkazi wa Gongo la Mboto.
HAITIBU KISUKARI
Licha ya dawa hiyo ya Babu kuaminika kuwa inatibu magonjwa kadhaa sugu ukiwemo wa kisukari, imeelezwa kuwa hadi sasa hakuna dawa iliyothibitishwa kitaalam kuwa na uwezo wa kutibu maradhi hayo.
“Kwa kifupi, hii ni aibu. Serikali haipaswi kuogopa kusema ukweli kuwa dawa ya Babu haitibu kisukari. Wote wanaosumbuliwa na ugonjwa huo nawaomba wasiache kutumia dawa za hospitali.
Wakifanya hivyo watapoteza maisha, najua kwa kusema hivi sasa mawaziri wapo matumbo moto, lakini huo ni ukweli,” alisema daktari mmoja wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambaye aliomba jina lake kuhifadhiwa kwa kuwa si msemaji.
Aliitaka serikali kusema ukweli juu ya hilo ili kuokoa maisha ya Watanzania wengi ambao wanaamini kisukari kinaponywa kwa kikombe cha Babu, hali inayofanya baadhi yao kuwa hoi kwa kuzidiwa na ugonjwa huo.
AINA MBILI ZA KISUKARI
Alifafanua kuwa, kuna aina kuu mbili za kisukari kama wataalam wa tiba walivyoweza kuzigawa. Aina ya kwanza ni kisukari ambacho mtu anakipata tangu wakati anazaliwa hadi anapofika umri wa miaka 35, ikamaanisha kuwa katika muda huo mtu anaweza akaugua kisukari.
Aina ya pili ni kile ambacho mtu hukipata anapofika umri wa miaka 40 na kwenda juu. Vile vile kuna kisukari humtokea mtu anapokuwa na mimba, akasema hicho huitwa kisukari cha mimba.
“Aina mbili za kisukari nilizoelezwa zina tiba zinazotofautiana. Mgonjwa anayepata kisukari cha kwanza hutakiwa kufuata miiko (kutokula vyakula vya sukari), kisha hutakiwa kuchoma sindano yenye dawa ya Insulin ambayo hufanya kazi ya kuiweka sukari ndani ya mwili katika kiwango kinachotakiwa.
“Mgonjwa wa kisukari wa aina hii hutakiwa kuchoma sindano ya Insulin mara mbili au tatu kila siku. Mara nyingi wagonjwa hufundishwa kujichoma wenyewe sindano au kwa watu walio karibu nao. Kutokana na hayo, sikuona sababu ya serikali kutongoja uchunguzi wa kisayansi kuhusu dawa ya Babu kabla ya kuiruhusu kutumika,” alisema daktari huyo.
MAJIBU YA WAZIRI BUNGENI
Akijibu swali bungeni katika kikao cha bunge kilichopita mjini Dodoma , Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Lucy Nkya alisema kuwa, hadi sasa tafiti za kitaalam zilizofanywa nchini na duniani zimeonesha kuwa, dawa zote zilizopo pamoja na za asili zina uwezo wa kudhibiti ugonjwa usisababishe madhara zaidi lakini hazina uwezo wa kuponyesha kabisa.
“Katika mfumo wa tiba asilia, kuna dawa nyingi zinazotumika kudhibiti ugonjwa wa kisukari mwilini kama ilivyo katika mfumo wa tiba za kisasa. Wizara kupitia Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) na Taasisi ya Tiba Asili ya Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba ya Jamii Muhimbili, hufanya tafiti mbalimbali za dawa asili zinazosadikiwa kutibu magonjwa mbalimbali ikiwemo kisukari.
Matokeo ya tafiti hizo hayajaonesha dawa yoyote ya asili yenye uwezo wa kutibu kisukari,”alisema Dk. Nkya.
Dk.Nkya ambaye alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kidawa Hamisi aliyetaka kujua tamko la serikali kuhusiana na wimbi la waganga wa tiba za asili wanaojitangaza kutibu ugonjwa wa kisukari, alisema kuwa dawa inapotangazwa kwenye vyombo vya habari lazima iwe imefanyiwa utafiti wa kitaalam na kuthibitishwa kuwa ina uwezo wa kutibu, kinyume chake ni uvunjwaji wa sheria namba 23 ya mwaka 2002 kuhusu tiba mbadala na kanuni zake.
Alisema wataalam wa miti shamba kabla ya kutangaza hizo dawa zao kwa umma wanapaswa wawasiliane na waganga wakuu wa wilaya na mikoa ili taratibu za kuzifanyia dawa hizo utafiti wa kisayansi zifanyike.
Dk.Nkya aliitahadharisha jamii kuhusiana na dawa hizo asili zinazotajwa kutibu ugonjwa wa kisukari kuwa hazitibu zaidi ya baadhi kuthibitika kuudhibiti ugonjwa na kwamba wananchi wajenge tabia ya kwenda kuchunguza hali ya afya zao mara kwa mara ili kuwezesha kudhibiti ugonjwa mapema.
Hata hivyo, uchunguzi wetu umebaini kuwa licha ya majibu hayo mazuri ya naibu waziri huyo, hivi sasa serikali imekuwa ikiacha watu, wakiwemo mawaziri na wafanyabiashara mbalimbali wakienda kwa Babu Loliondo na kunywa dawa ambayo bado haijathibitishwa kisayansi kama inatibu magonjwa yanayotajwa.
Wakati huo huo, viongozi mbalimbali wa serikali wamelaumiwa na wananchi kwa kitendo chao cha kwenda kwa Babu kwa ‘mgongo’ wa serikali kumbe wana nia ya kunywa dawa.
Baadhi ya wananchi waliozungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti walisema viongozi wa serikali wakiwemo mawaziri, wakuu wa mikoa, majaji, wakuu wa wilaya na hata makamanda wamekunywa dawa ya babu kwa kutokaa kwenye foleni.
“Mara baada ya kufika nyumbani kwa Mchungaji Masapila, huwa wanaandaliwa eneo maalum na hujifanya wana mazungumzo ya kiserikali lakini baadaye kila mmoja hupata kikombe cha dawa, na kuwaacha wananchi kwenye foleni. Hili ni kosa kubwa kabisa kiimani,” alisema mwananchi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Aloyce Ngongoa.
Baadhi ya mawaziri waliopata kikombe kwa Babu wa Loliondo ambao picha zao zipo ukurasa wa mbele wa gazeti hili ni William Lukuvi, Steven Wassira, John Magufuli, Teresya Hovisa na Wakuu wa Mikoa Abbas Kandoro, Yohana Balele, mtoto wa baba wa taifa, Rose Nyerere na Mbunge Nimrodi Mkono.
Wengine ni Augustino Mrema, mawaziri wakuu wa zamani, Edward Lowassa, (pichani) Frederick Sumaye, Mkuu wa Wilaya, Edmund Mjengwa na viongozi wengine wa chama na serikali.
Raia wa kigeni
Mamia ya raia wa kigeni kutoka nchi mbalimbali duniani nao wamekuwa wakimiminika katika Kijiji cha Samunge kupata tiba ya magonjwa mbalimbali.
Kwa mujibu wa takwimu zinazokusanywa katika eneo la utoaji wa dawa, raia hao wa kigeni wametoka Kenya, Marekani, Finland, Uholanzi, Sri Lanka, Jumuiya ya Falme za Kiarabu (UAE), Malawi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC), Uganda, Rwanda, Burundi na Comoro.
Nayo Idara ya Uhamiaji tayari imepeleka ofisa wake ambaye ameweka kambi Samunge kupitia nyaraka mbalimbali za wageni wanaoingia kijijini hapo kunywa dawa.
Comment
Comment by erick john on April 26, 2011 at 1:16pm Hii inahusiana na imani. Kuwa na imani uishi/kosa imani ufe!!
Comment by tanzanian boy on April 23, 2011 at 5:25pm
Comment by Lutchiana Robert on April 9, 2011 at 12:39pm
Comment by juan son miguel on April 8, 2011 at 10:11pm
Comment by Nurudin Iddi Kassim on April 8, 2011 at 5:06pm kilam2afanye afikirie swala babu baade utapaata chakufany ni nn kwa mtazamo wako
Comment by Herieth leonard on April 8, 2011 at 3:16pm
Comment by Ashagrace on April 8, 2011 at 10:02am
Comment by benny tungaraza on April 7, 2011 at 11:54am
Comment by tanzanian boy on April 6, 2011 at 5:19pm | 1 |
GLOBAL |
| 2 |
julius manning |
| 3 |
Man KKK |
| 4 |
Sili Silali |
| 5 |
IL-YA |
| 6 |
chama baby |
| 7 |
msichoke mlugu |
| 8 |
kaka |
| 9 |
Maji Marefu |
| 10 |
Kelvin Luhala Eto'o |
othman Ochu posted a status
mrembo commented on Sili Silali's photo

You need to be a member of Global Publishers to add comments!
Join Global Publishers