Na Ashe Hassan
Mtoto Subira Ally (12), Mkazi wa Kijiji cha Malema, Kata ya Maratani, wilayani Nanyumbu, mkoani Mtwara ameonekana kumpindua Babu wa Loliondo, Mchungaji Ambilikile Masapile (pichani) kwa kupata wateja wengi ambao wanakwenda kutibiwa.

Kupinduliwa kwa Babu kumetafsiriwa na watu baada ya kuonekana sasa nyumbani kwake Kijiji cha Samunge hakipati wageni wengi kama ilivyo Kijiji cha Malema anakokaa Subira ambako  wageni kutoka mikoa mbalimbali na nchi jirani hufurika kila kukicha.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni, mtoto Subira alisema kuwa siku moja ,  Aprili mwaka huu akiwa amelala alioteshwa ndoto iliyokuwa ikimuelekeza kuwa anatakiwa atoe tiba kwa njia ya kikombe kwa kutumia mzizi wa mti uitwao Mkong’oto unaopatikana hapo nyumbani kwao, hivyo kumjulisha mama yake mkubwa anayeishi naye.

“Niliambiwa kuwa dawa hiyo itakuwa inatibu Ukimwi, kisukari, kuponya vipofu, viziwi, na wote ambao miili yao itakuwa imekufa ganzi au kupooza,” alisema Subira.

Aliongeza kuwa dawa hiyo ya kikombe alioteshwa kuwa iwe ikinunuliwa kwa gharama ya shilingi 500. Alipoulizwa ni watu wangapi ambao amewatibu tangu alipoanza kazi hiyo alisema ni wengi sana.

“Wagonjwa ni wengi sana ambao wamepata kikombe na wanaendelea kufika hapa nyumbani,” alisema huku akiwa na mama yake mkubwa aliyefahamika kwa jina moja la Binti Ismail.

WAGENI TOKA NJE YA NCHI


Subira alisema licha ya kutibu wananchi wa Tanzania, amekuwa akipokea wageni wengine kutoka nje ya nchi kama vile Msumbiji na Malawi.

Aliongeza kuwa licha ya wagonjwa wengi kutoka Tanzania bara, amepokea wengine kutoka  Visiwani Zanzibar na anakumbuka mmoja alikuwa na matatizo ya miguu ambayo ilikuwa imekufa  ganzi kwa miaka mitano. “Sasa mgonjwa huyo wa Zanzibar ganzi imekwisha na anatembea vizuri, amemshukuru sana Mungu.” Mama mkubwa wa binti huyo, aliyefahamika kwa jina la Binti Ismaili alithibitisha mwanaye kuoteshwa na kutoa tiba hiyo.

MASHUHUDA

Naye mama mmoja  aliyejitambulisha kwa jina moja tu la Sharifa  mkazi wa Tandika Mikoroshini  jijini Dar es Salaam aliyezungumza na mwandishi wetu hivi karibuni alisema kuwa, alikuwa muathirika wa ugonjwa wa Ukimwi lakini baada ya kutumia dawa ya mtoto huyo na kwenda kupima ameonekana hana virusi vya maradhi hayo.

“Baada ya kutumia dawa ya Mkong’oto nimepona,nilikwenda kupima katika Hospitali ya Maratani mkoani Mtwara  na kuthibitishiwa na daktari aliyenipima aitwae Dk.Namihambi  kuwa sina virusi. Nangoja kupima mara ya pili kwa uhakika zaidi,” alisema.

Aidha, baba mmoja ambaye aliomba jina lake kuhifadhiwa alisema kuwa alikuwa na ugonjwa wa Ukimwi lakini sasa hana baada ya kupimwa katika Hospitali ya Mkomaindo, Masasi.

WAZIRI WA AFYA ALICHOSEMA

Mara baada ya Babu Masapile kutangaza kuoteshwa kutoa tiba ya magonjwa sugu, watu wengi wameibuka kutoa tiba hiyo na wananchi kufurika kupata kikombe.

Hata hivyo, wiki iliyopita gazeti hili lilimkariri Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hadji Mponda akisema kuwa katika tafiti za kitaalamu dawa za mitishamba hazijathibitishwa kutibu Ukimwi.

Kauli hiyo ilitolewa na waziri huyo wakati anazindua Kituo cha Matibabu ya Wagonjwa wa Ukimwi na Mafunzo katika Hospitali ya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.

Dk. Mponda alisema wagonjwa wa Ukimwi wanatakiwa kutumia dawa za kurefusha maisha (ARV) na akawataka waende kwenye vituo vya afya kupewa.“Wagonjwa wanaokwenda kupata tiba asili waache kwa kuwa bado zinafanyiwa utafiti,” alisisitiza Waziri Mponda.

Views: 814

Tags: uwazi11

Comment

You need to be a member of Global Publishers to add comments!

Join Global Publishers

Comment by baraka ndesamburo on August 9, 2011 at 5:07pm
kweli wonders shall never end na WAJINGA NDIA WALIWAO
Comment by uba jumanne salim on August 6, 2011 at 11:27pm
no koment kwa kweli na hii ni kwa sababu huyo ni mtoto ,mi napita tu
Comment by mawanipk on August 6, 2011 at 6:54pm

jamani  tuache utani na maisha  tamaa  za pesa hizi zitatupeleka  kuzimu

baada ya babu ni vikombe vingapi vimetokea na  wako wapi?????????????????????

akiota  tu usiku asubuhui anasema niemoteshwa  je huyo mungu wenyewe wanamfahamu ?????????

Comment by DINA FLAMINGO on August 6, 2011 at 2:36pm
hebu acheni masihara msione kitu
Comment by mawanipk on August 5, 2011 at 7:19pm
naam twende kazi kama mimi naja na kombe langu
Comment by simon paul on August 5, 2011 at 6:21pm

duuhh.. hii sasa ni kopi to pesti mana kati pasti haitaleta maana...!!! hizi ndoto ni mpaka liniii...?

 

Comment by Luchius Protas on August 4, 2011 at 11:11pm
Copy na dublicate vyote sawa. Original ni moja tu, BABU wa Samunge
Comment by gladsn naftal on August 4, 2011 at 11:16am
haya  tenah .............
Comment by sophy on August 4, 2011 at 9:36am
Hizi ni dalili za siku za mwisho Ilikuwa Babu, Bibi na sasa mtoto "Tujiandae"
Comment by rf on August 3, 2011 at 9:57pm
siamini kama watanzania tunakuwa wajinga kiasi hiki ni umasikini au elimu jamani........................


ADVERTISEMENT


TANGAZA HAPA

ADVERTISEMENTS

Latest Activity

GUNZ TRUVADA posted a status
"KUMPA ASIYE KUPA NI SAWA SAWA NA KUTUPA"
2 minutes ago
othman Ochu posted a status
"SCENE 1 WAHUSIKA: AMIDU , SHARIFA MAHALI: ZANZIBAR MUDA : JIONI ( WAKIWA WANASHUKA TOKA KATKA BOTI YA JION KUINGIA KATKA MJI WA ZANZI"
9 hours ago
Priscus Adelard shared GLOBAL's blog post on Facebook
9 hours ago
mrembo commented on julius manning's photo
Thumbnail

Mtanzania huru

"pole sana usijali iko siku mungu atakujaalia mungu hamtupi mja wake"
10 hours ago
mrembo commented on Sili Silali's photo
Thumbnail

Duh!

"mama mzima hayawani mavazi gani hayo takupa mfano chungwa likiwa halijamenywa unatamani ulile…"
10 hours ago
kaka commented on Ali Amur Ali's video
Thumbnail

AZIMIO LA KUANGAMIZA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE

"hapo ni kina dada kutua comment zao"
10 hours ago
Gaston Kayombo commented on Ali Amur Ali's video
12 hours ago
roylicious and Jackson Jacob are now friends
12 hours ago
babu wa loliondo (cup) updated their profile
12 hours ago
julius manning commented on julius manning's photo
Thumbnail

vijana 2016 itakuwa hivi

"@furaha mimi ni kikongwe hayo ni kazi kwako."
13 hours ago
Masalu Mayeji Many'hasimha shared GLOBAL's blog post on Facebook
13 hours ago
kheri zewe commented on Sili Silali's photo
Thumbnail

Duh!

"minyama uzembe"
13 hours ago

© 2012  

Designed & Developed by
G5 CLICK COMPANY.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service

How to make a Website