All News Posts Tagged 'hadithi11' (1,493)

THE DIRTY GAME (MCHEZO MCHAFU) - 12

MAUAJI ya mfululizo ya wafanyabiashara maarufu wa madini yanawachanganya mno polisi wa Tanzania na Kenya. Wingu la sintofahamu linazidi kutanda huku polisi wakijitahidi kwa kadiri ya uwezo wao kumtafuta mhusika.

Mauaji ya kwanza yalikuwa ni ya Hans Kekule, mfanyabiashara aliyeuawa na msichana mdogo, Cecilia kwa kuchomwa kisu kwenye maadhimisho ya kilele cha Siku ya Maonesho ya Biashara maarufu kama Sabasaba.

Baada ya tukio hilo, msichana huyo…

Added by GLOBAL on May 22, 2013 at 9:00am — 3 Comments

Raymond and Stephanie Raymond na Stephanie -84

MSAFARA wa magari yasiyopungua hamsini ulielekea kwenye Makaburi ya Miami Cemetery, mahali ambako ndiyo ungekuwa mwisho wa safari ya kijana Martin Morris Jnr aliyekuwa amefariki dunia kwa kuipigania nchi yake ya Marekani. Kwao ilikuwa ni siku mbaya kuliko zote zilizowahi kutokea.

Kwa takribani saa moja, msafara huo bado ulikuwa barabarani, hatimaye ukawasili makaburini, watu wakaanza kuteremka kuingia ndani ya eneo la makaburi.

Stephanie…

Added by GLOBAL on May 22, 2013 at 8:00am — 5 Comments

Termination of the World (KUANGAMIA KWA DUNIA-77)

AHADI ya siku nyingi aliyoiweka Nsia ya kuuangamiza ulimwengu, sasa inaelekea kutimia. Msichana huyo hatari anayesumbua vichwa vya watu wengi kutokana na matendo yake ya kikatili, baada ya kurejea Tanzania akitokea Israel anaanza kutimiza ahadi yake. Anamwaga sumu ya Carcinoma Powder kwenye kijiji alichozaliwa cha Hedaru na kusababisha maafa makubwa.

Baada ya kufanya unyama huo, Nsia anaelekea kwenye mtambo wa kusafisha na kuchuja maji wa Ruvu unaotegemewa na…

Added by GLOBAL on May 21, 2013 at 8:00am — 7 Comments

KUMBUKUMBU ZA KWELI ZA MAISHA YA SHIGONGO - 31

SAFARI yangu ya maisha imenifikisha Kisiwani Zanzibar, nikiwa na rafiki yangu Muitaliano aitwaye Mariano Covre kutoka Verona. Huyu alikuwa mtalii niliyekutana naye Bagamoyo na kuwa marafiki wakubwa, akanichukua kama mtu wa kusafiri naye kuelekea Zanzibar kwa sababu alikuwa hawezi kuongea Kiswahili. Kazi hii niliifanya kwa malipo ya shilingi mia tano kwa siku.

Tukiwa Dar es Salaam, tulikutana na msichana wa Kimarekani, Patricia. Huyu akaungana nasi katika safari…

Added by GLOBAL on May 20, 2013 at 9:30am — 6 Comments

HEART ATTACK (SHAMBULIO LA MOYO) - 9

ILIPOISHIA:

“JAMANI huyo siyo mwizi, nisikilizeni, siyo mwizi jamani,” alisema Alphonce huku akisaidiwa na yule dereva wa bodaboda, wakawasukuma wale watu na kwenda mpaka pale Brighton alipokuwa amelala akiwa hajitambui.  Wakawaelewesha wale watu kila kitu kilichotokea.  Kila mtu akaanza kumlaumu yule msichana kwa kitendo alichokifanya lakini tayari walikuwa wamechelewa, Matilda alishapotea eneo lile.

SASA ENDELEA…

IKABIDI…

Added by GLOBAL on May 20, 2013 at 9:00am — 3 Comments

THE DIRTY GAME (MCHEZO MCHAFU) - 11

WINGU la sintofahamu linazidi kutanda kwenye nchi za Tanzania na Kenya baada ya mfululizo wa mauaji ya wafanyabiashara maarufu wa madini.

Wa kwanza kuuawa alikuwa ni Hans Kekule, aliyeuawa kwa kuchomwa kisu kwenye maadhimisho ya kilele cha Siku ya Maonesho ya Biashara maarufu kama Sabasaba na msichana mdogo, Cecilia.

Baada ya tukio hilo, msichana huyo anahukumiwa kunyongwa hadi kufa. Baada ya kusota miaka mingi gerezani akisubiri siku yake…

Added by GLOBAL on May 20, 2013 at 9:00am — 4 Comments

Queen of the Gorillas (Malkia wa Masokwe) - 112

NDOA ya Harrison na Angel, msichana aliyemhangaikia sana kabla ya kumpata na kumuoa, inazidi kushamiri huku upendo, heshima na maelewano vikizidi kuongezeka kila kukicha.

Upande wa pili, msichana ambaye Harrison alimkimbia siku ya harusi yao, Linda ameamua kulivalia njuga suala la kutoweka kwa mpenzi wake huyo na baada ya kusomea upelelezi kwa kipindi kirefu na kufuzu, anaanza kumfuatilia hatua kwa hatua akitaka kujua yuko wapi na anafanya…

Added by GLOBAL on May 20, 2013 at 9:00am — 10 Comments

Raymond and Stephanie Raymond na Stephanie -83

Baada ya kuthibitishiwa kwamba kweli Martin hakuwepo tena duniani, familia ya mzee Morris inaangua kilio, hakuna ambaye yupo tayari kukubaliana na tukio hilo gumu maishani. Stephanie, mama wa Martin wanaangua kilio huku wakimwita Martin arejee tena.

Madaktari na wauguzi wanatumia muda huo kuwasihi na kuwabembeleza kwamba  ilikuwa ni lazima wakubaliane na taarifa hizo  kwani huo ndiyo ulikuwa ukweli.

“Unajua wewe ni mwanaume, jikaze…

Added by GLOBAL on May 18, 2013 at 10:00am — 2 Comments

Queen of the Gorillas (Malkia wa Masokwe) - 111

WAKATI mapenzi kati ya Harrison na Angel yakizidi kupamba moto, wakimshukuru Mungu wao kwa kuwaongezea furaha kwa kuwajalia kupata mtoto mzuri wa kiume, Harvey Junior, kumbe Linda anafanya kila liwezekanalo kuingia kwenye maisha yao.

Baada ya kufanikiwa kufahamu nyumba waliyokuwa wanaishi Harrison na mkewe, jioni moja Linda anaenda nyuma ya nyumba hiyo na kusikiliza mazungumzo ya wanandoa hao. Anasikia wakizungumzia kuhusu kutafuta hausigeli.…

Added by GLOBAL on May 17, 2013 at 8:58am — 12 Comments

THE SECRET AGREEMENT - 11

ILIPOISHIA...

Alikazana hadi alipokutana na Barabara ya Tunisia inayoelekea Mbuyuni kupitia Kiwanda cha Kahawa cha Coffee Quring na ile inayopandisha kwenda Kwa Kishamba.

SASA ENDELEA...

AKASHIKA ya kulia kwake. Hakuuachia mwavuli wake ambao ulimsaidia sana kuzuia mvua iliyoendelea kunyesha. Dakika tatu baadaye alikuwa ameshafika Kwa Kishamba. Kama alivyoelekezwa na Zakhia, alizunguka nyuma ya Zahanati hiyo na kwenda kusimama…

Added by GLOBAL on May 17, 2013 at 8:00am — 3 Comments

The End of Torture (Mwisho wa Mateso) - 27

MAFURU, mwanaume wa makamo anamgeuza Amelia, msichana ambaye kiumri alikuwa sawa na mwanaye wa kumzaa kuwa mtumwa wa ngono. Anatumia udhaifu wa matatizo yaliyomsibu msichana huyo baada ya kufiwa na wazazi wake kuwa kama mtaji wake. Awali alijifanya msamaria mwema, lakini baada ya kuzoeana na Amelia, alitumia mbinu zote mpaka akatimiza haja zake.

Akawa anamtumia kingono msichana huyo karibu kila siku huku akimrubuni kwa misaada ya fedha na zawadi ndogondogo. Awali…

Added by GLOBAL on May 16, 2013 at 8:30am — 6 Comments

THE DIRTY GAME (MCHEZO MCHAFU) - 10

MSHTAKIWA Cecilia aliyekutwa na hatia ya kumuua mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania, Hans Kekule, anazua gumzo baada ya kuamua kuyakatisha maisha yake akiwa gerezani wakati akisubiri siku ya hukumu ya kunyongwa. Anajibamiza ukutani kwa nguvu na kujipasua kichwa baada ya kuchoshwa na kile alichokiita kucheleweshwa kwa hukumu yake kwa makusudi.

Licha ya msichana huyo kuzikwa na Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na jiji, bado anaonekana kwenye tukio lingine la…

Added by GLOBAL on May 15, 2013 at 10:22am — 8 Comments

HEART ATTACK (SHAMBULIO LA MOYO) - 8

Na Hashim Aziz

ILIPOISHIA:

Wakiwa wanajiandaa kuingia kwenye mpambano wa kirafiki usio na jezi wala mwamuzi, wote walishtuka kupita kiasi kusikia mlango wa chumba cha Alphonce ukigongwa kwa nguvu. Kwa bahati mbaya zaidi, Alphonce hakukumbuka hata kufunga mlango huo alipoingia na Matilda, wote wakashtukia mtu akiingia kwa kasi ndani, wakabaki kubabaika kwa aibu kwani hakuna aliyetegemea jambo hilo kutokea.

SASA…

Added by GLOBAL on May 15, 2013 at 9:30am — 4 Comments

Raymond and Stephanie (Raymond na Stephanie) - 82

HALI ya Martin ni mbaya pamoja na kwamba bado anapumua, yuko ndani ya chumba cha wagonjwa mahututi na tumaini la kupona halipo kwani majeraha yake ni makubwa na uchunguzi wa madaktari umethibitisha kwamba ameungua asilimia sabini ya mwili wake.

Pamoja na yote, bado madaktari wanajitahidi kujaribu kuokoa maisha ya kijana huyu mdogo ambaye ametokea kujipatia umaarufu kwa muda mfupi tu tangu aanze kazi ya urubani.

Wakati  matibabu…

Added by GLOBAL on May 15, 2013 at 8:30am — 6 Comments

Termination of the World (KUANGAMIA KWA DUNIA-76)

NSIA anataka kutimiza ahadi yake ya kuiangamiza dunia. Msichana huyo hatari anayesumbua vichwa vya watu wengi kutokana na matendo yake ya kikatili, baada ya kurejea Tanzania akitokea Israel anaanza harakati za kutimiza ahadi yake. Chuki na hasira zake zinatokana na mateso anayoyapata ya kusumbuliwa na nguvu za giza ambazo wazazi wake walikuwa wakizitumikia.

Pigo la kwanza analiangushia kwenye kijiji alichokuwa anaishi na wazazi wake pamoja na ndugu zake wengine…

Added by GLOBAL on May 14, 2013 at 9:30am — 5 Comments

THE DIRTY GAME (MCHEZO MCHAFU) - 9

MSICHANA Cecilia aliyefanya tukio la kutisha la kumchoma kisu na kumuua aliyekuwa mgeni rasmi wa maadhimisho ya Sikukuu ya Maonyesho ya Biashara, Sabasaba, Hans Kekule, anahukumiwa kunyongwa na kupelekwa kwenye Gereza la Segerea kusubiri siku yake ya kutiwa kitanzi.

Anakaa gerezani kwa miaka saba bila kutekelezwa kwa hukumu yake, jambo linalomfanya ajipigize ukutani kwa nguvu hadi mauti yanapomkuta. Baada ya kuzikwa na kila mmoja kuanza kusahau kuhusu matukio…

Added by GLOBAL on May 13, 2013 at 9:00am — 6 Comments

True Memories Of My Life [Kumbukumbu za Kweli za Maisha Ya Shigongo] - 29

Nimeshaeleza kuhusu elimu yangu, mateso niliyoyapata maishani mimi na familia yangu, nilivyopuuzwa na asilimia kubwa ya watu ambao waliamini mtu kama mimi, kutoka familia kama yangu asingeweza kufanya jambo lolote la maana maishani! Kazi yangu kubwa ilikuwa kupigana vita ya maisha ili nije kuwaonesha watu hao kwamba kile walichokifikiria juu yangu, kilikuwa ni uongo.

Nimefika mahali ambako ninasoma Chuo cha Uganga Kilosa, nikiwa kijana mdogo wa miaka ishirini.…

Added by GLOBAL on May 13, 2013 at 9:00am — 6 Comments

Queen of the Gorillas (Malkia wa Masokwe) - 110

MAHABA ya dhati yanazidi kushamiri kwenye ndoa ya Harrison na mkewe Angel. Mungu anawajalia kupata mtoto wa kwanza wa kiume, Harvey Junior, jambo linalozidisha mapenzi. Kila mmoja anaifurahia ndoa na hakuna anayejuta kukutana na mwenzake.

Kupitia kidani alichokuwa amekivaa Angel tangu Harrison amfahamu, wanagundua kuwa kuna majina matatu yameandikwa. Harrison anakipeleka kwa sonara na kugundua kidani kina majina ya Charlote Abdulkarim Charwe. Anaanza kupeleleza…

Added by GLOBAL on May 13, 2013 at 8:30am — 11 Comments

Raymond and Stephanie Raymond na Stephanie -81

UMATI mkubwa wa watu uliofurika kwenye hospitali ya jeshi ukawa na shauku kubwa ya kuwaona ndugu zao, wakiwa hai au wamekufa. Kila mmoja akawa anasubiri kutangaziwa utaratibu wa kuanza kwa kazi ya kuwatambua ndugu zao.

Baada ya muda, ndugu zake Martin wanapata taarifa kuwa kijana huyo alikuwa amepelekwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi (ICU) kutoka na hali yake kuwa mbaya. Baada ya utaratibu maalum kufuatwa, mzee Morris anawaongoza mkewe na Stephanie mpaka kwenye…

Added by GLOBAL on May 11, 2013 at 7:54am — 3 Comments

THE DIRTY GAME (MCHEZO MCHAFU) - 8

MAADHIMISHO ya Sikukuu ya Maonyesho ya Biashara, Sabasaba yanaingia doa baada ya msichana mdogo, Cecilia kuvamia sherehe hiyo na kwenda kumchoma kisu shingoni mfanyabiashara maarufu, Hans Kekule ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi.

Damu inatapakaa kwenye meza aliyokuwa amekaa mgeni rasmi na maadhimisho ya sherehe hizo zilizokuwa zinafanyika kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam yanavurugika. Baada ya kutekeleza unyama huo, Cecilia anajaribu…

Added by GLOBAL on May 10, 2013 at 8:30am — 7 Comments

ADVERTISEMENT


Advertisement

 

Forum

KIPIGO CHA BAO 2-1 KWA MAN UTD, KOSA LA MWAMUZI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Mohammed Mar 26. 6 Replies

JE, NI KWELI KWAMBA KIPIGO CHA BAO 2-1 ILICHOKIPATA MAN UTD KUTOKA KWA REAL MADRID USIKU WA KUAMKIA LEO LAWAMA ZOTE ZIMWENDEE MWAMUZI WA MCHEZO AU MAN UTD WAJILAUMU WENYEWE? TUPE MAONI YAKO!!!

HALI INAYOENDELEA BUNGENI, SPIKA NA NAIBU WAKE WAMESHINDWA KUONGOZA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Ali Abdalla Ali Apr 22. 20 Replies

Tumeshuhudia kwa siku za hivi karibuni hali halisi iliyokuwa inatokea katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, kwa hali hii ni ishara kuwa Spika na Naibu wake washindwa kuliongoza bunge hilo?

VURUGU ZA CCM NA CHADEMA KUGOMBEA MLINGOTI WA BENDERA DODOMA, NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Phinehas Rishiansia Kileo May 3. 6 Replies

Wafuasi wa CCM wakimshambulia mfuasi wa Chadema mkoani Dodoma…

Tags: BENDERA, WA, DODOMA, NANI, KULAUMIWA?

VURUGU ZINAZOENDELEA HAPA NCHINI NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by NELSON UVAMBE on Monday. 27 Replies

HIVI KARIBUNI KUMEKUWEPO UPOTEVU WA AMANI HAPA NCHINI PAMOJA NA WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI. MKOANI KAGERA WANANCHI WENYE HASIRA WALIWAUA POLISI, IJUMAA ILIYOPITA WAKULIMA NA WAFUGAJI HUKO WILAYANI KILOSA WALIZUA VURUGU NA KUFUNGA BARABARA,…

MRISHO NGASSA KUPELEKWA SIMBA SC BILA RIDHAA YAKE, JE NI HALALI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Domino Bagambisa Jan 21. 17 Replies

Kiungo hatari wa Azam FC, Mrisho Ngassa leo amepelekwa Simba SC kwa mkopo na timu yake…

Tags: SOKA

hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Started by Gysper in Siasa. Last reply by Jamal amor May 9. 24 Replies

 hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Kauli Ya JK kuwa Mauaji ya Arusha ni "Bahati Mbaya"

Started by Kulikoni Ughaibuni in Siasa. Last reply by richardngeze Feb 12. 12 Replies

Tanzania tuna tatizo kubwa.Hakuna haja ya kunyoosheana vidole as to nani amechangia tatizo hilo bali cha muhimu na haraka ni namna tutakavyoweza kutatua tatizo hili.Nisimung'unye maneno: tatizo kubwa linaloikabili ni kuwa na Rais ambaye takriban…

Latest Activity

tina babi left a comment for Prince Mayer
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
30 seconds ago
tina babi left a comment for JOSEPH MNANGU
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
41 seconds ago
tina babi left a comment for mtola mtola
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
1 minute ago
tina babi left a comment for shiller mc mpanda
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
1 minute ago
tina babi left a comment for daniel
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
3 minutes ago
tina babi left a comment for daniel
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
4 minutes ago
tina babi left a comment for MAHIR EMMA
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
4 minutes ago
tina babi left a comment for mugisha omary
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
4 minutes ago
tina babi left a comment for good boy
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
4 minutes ago
tina babi left a comment for babo hussantino gou
"tinalutunku@yahoo.comHello,My name is Miss tina lutunku.i saw your profile today and become…"
5 minutes ago
tina babi left a comment for babo hussantino gou
5 minutes ago
Alvin Falk posted a status
5 minutes ago

© 2013   Created by Global Publishers.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service