UKUMBI WA KISLAMU

Information

UKUMBI WA KISLAMU

huu ukumbi ni wakupeana mawazo na kuelimishana mambo ya mungu munakaribishwa walio waislamu na wale ambao si waislamu mambo ya mungu hayana ubaguzi karibuni

Location: KENYA
Members: 86
Latest Activity: May 10

Discussion Forum

TAREHE 10 MUHARRAM HAPO KARBALA:Haya ndio yaliyotokea -2-.

Started by Hussein Marandu Nov 28, 2012. 0 Replies

MASAHABA WAINGIA UWANJANI:Masahaba wa Imam Hussein(a.s) hawakua watu wa kawaida.Hawa ni masahaba wa Mtume(s.a.w.w),wa Imam Ali(a.s),wapenzi wa Mtume na kizazi chake kilichotoharishwa.Walikua…

TAREHE 10 MUHARRAM HAPO KARBALA.Haya ndiyo yaliyotokea:-1-

Started by Hussein Marandu Nov 27, 2012. 0 Replies

Wasomaji wenye utambuzi,Asalaam alaykum.TUNAPOREJEA kurasa za historia,tarehe 10 Muharram,ni siku ya kipekee isiyo na kifani,siku iliyochana pazia za giza na kuacha nuru kuchomoza na kuwajaza upya…

ASHURA:Mtizamo wa Kihistoria Sehemu ya Kwanza

Started by Hussein Marandu Nov 15, 2012. 0 Replies

TUZIREJESHE AMANA KWA WENYEWE NA TUHUKUMU KWA UADILIFUMwenyezi Mungu anasema:"Mwenyezi Mungu anakuamrisheni mzirejeshe amana kwa wenyewe.Na mnapohukumu baina ya watu,basi hukumuni kwa uadilifu.Hakika…

ASHURA:Mtizamo wa Kihistoria.

Started by Hussein Marandu Nov 13, 2012. 0 Replies

UTANGULIZI:SIFA zote njema ni zake Mwenyezi Mungu Bwana wa viumbe wote.NAMPENDA Mtume (s.a.w.w) alochaguliwa,na binamu yake Ali(a.s), na wajukuu wake wawili na Fatima Zahraa.WAO ndio AHLUL BAYT ambao…

Comment Wall

Comment

You need to be a member of UKUMBI WA KISLAMU to add comments!

Comment by Hashim.Makusi on February 26, 2013 at 5:56pm

Asalaam Aleykum,

Namshukuru mwenyezi mungu kwa kunijalia kuliona kundi na kujiunga ili niweze kupata faida leo hii hapa duniani na kesho akhera Inshaallah!

Comment by Al-Barry on February 25, 2013 at 12:32am
Assalamu Alaykum!
Namshukuru Allah kwa kuniruzku siha na afya njema nikiwa katika neema adhimu ya Uislamu!

Naam! Napenda kutoa shukurani zangu za dhati kwa uongozi mzima wa ukumbi huu mubaarak! Kwa kunikubalia ombi langu la kujiunga nao ili kupata faida kutoka kwa Mashekhe wetu waliomo ukumbini.

Namuomba Allah anijaalie kua msikilizaji mwema....washukran
Comment by maryam soud sleiman on February 18, 2013 at 1:44pm

s.alaykum ndugu zangu wa kiislam nimefurahi sana kuona hii grp na inshaallah Allah atukupeni kila la kheri,

Comment by Karim Abedi on November 16, 2012 at 2:23pm
HUU NI MWAKA MPYA WA KIISLAMU NAWATAKIIA HERI WOTE AMBAO UMEWAFIKIA NA KUWAOMBEA DUA NJEMA WALE AMBAO HAWAKUBAHATIKA KUUFIKIA
Comment by Salim Nassor on November 9, 2012 at 9:49am

Assalam alaykum warahmatullahi taala wabaraqatuh.

Comment by Mohammed on September 26, 2012 at 3:35pm

Nimejiunganikakuta Segment hii kwa kweli nimeipenda Allah awazidishie vyote mlioko huku Amin

Comment by Hussein Marandu on September 3, 2012 at 3:56pm
Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehma,Mwenye Kurehemu.
Rehma na Amani zimshukie Kipenzi cha Mwenyezi Mungu,Bwana Wetu na Muombezi wetu Mtukufu Mtume na aali zake wema walotakaswa wakatakasika,na wote wanaofuata nyayo zao.
Enyi Waislam watambuzi,
Asalaam alaykum.

Tarehe 8 August 2012,dada yetu Khadija Ngayoma aliandika:
"Nimefiwa na mzazi wangu,inaruhusiwa kumtolea fitri?"
Mosi,nikupe pole sana kwa kufiwa na mzazi wako.Hii ndo njia yetu sote.Nimeona nimjibu dada yetu huyu kama ifuatavyo:
Ikiwa mzazi wako alikua anadaiwa fitri wakati wa uhai wake,yaani aliwajibika kulipa lkn hakulipa,basi una wajibu wa kumlipia.

Ila ikiwa hakua na deni lolote la fitri,HAIRUHUSIWI baada ya kufariki kwake kumlipia.Natumai utakua umenielewa vizuri vinginevyo upo huru kuuliza tena maana hapa tunaeleweshana na kupeana maarifa.Allah Mtukufu Anajua Zaidi.
Comment by Khadija Ngayonga on August 18, 2012 at 12:57pm
Assalaam Aleykum ndugu zangu katika iman.Nimefurahi kujiunga na grp hii ya mambo ya dini.Natumai nitaelimika sana.swali langu,kwa mfano nimefiwa na mzazi wangu,inaruhusiwa kumtolea fitri?
Comment by bongo on April 9, 2012 at 9:58pm

 

Mama Yako Baada Ya Kifo Chake

Ndugu yangu mpendwa, jua Akurehemu Allaah ya kwamba, hakika kuwatendea wama wazazi wawili hakuishi kwa kifo chao, kwani imepokelewa Hadiyth kutoka kwa Abu Usaydi As-Sa'adiy amesema: "Wakati sisi tuko mbele ya Mtume, mara ghafla akamjia mtu mmoja kutoka kwa Banu Salimah akasema: "Ewe Mtume wa Allaah, je, kumebakia chochote katika wema kwa wazazi wangu wa kuwafanyia baada ya kifo chao? Mtume akasema: ((Ndiyo! Ni kuwaombea rahma kwa Allaah na kuwaombea msamaha na kutekeleza ahadi zao baada yao, na kuunga undugu ambao hauungwi kwa wao, na kuwaheshimu marafiki zao))

Wema kwa wazazi wawili unaendelea katika kizazi cha mwanadamu na kinachofuata baada yake, imepokelewa kutoka kwa Ibn 'Umar, amesema Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ((wafanyieni wema wazazi wenu, nanyi watoto wenu nao watajiheshimu))

Vile vile wema kwa wazazi wawili unazidisha umri (Akipenda mwenyewe Allaah) kwani imepokewa kutoka kwa Sahal bin Mu'aadh, ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Yeyote atakayewatendea wema wazazi wake wawili, kheri nyingi sana ni zake yeye, Allaah Atamzidishia umri wake))

Tunamuomba Allaah Atusaidie kuwafanyia wema wazazi na kuwatii na kuwafanyia Ihsani wakiwa hai na wakiwa wamekufa, na asitufishe isipokuwa pale atakapokuwa Yu radhi na sisi, na tunamuomba Allaah Azishushe Rahma na Baraka na Amani Zake kwa Muhammad na kwa ahli zake na Maswahaba.

Comment by Marlown Mwaisanila on April 5, 2012 at 2:18am
ni kweli kuongopa tena hasa kwa mzaha ni dhambi kubwa.
 

Members (86)

 
 
 

ADVERTISEMENT


Advertisement

 

© 2013   Created by Global Publishers.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service