Ni jambo lisilopingika kwa mtanzania yeyote mwenye akili kuwa umasikini wetu tulio nao kwa sasa sio wa mali bali ni wa viongozi. Maana kama ni mali Tanzania tuna mali nyingi sana kuliko nchi yoyote kusini mwa jangwa la sahara ukiondoa Afrika kusini. Hata wale wanaotetea na kusifia vyama vyao wanafanya hivyo kwa nidhamu ya woga tu mana wanajua wakionyesha misimamo yao waziwazi rungu la vyama vyao litawaponda vichwani mwao hivyo wanabaki wakisifia vyama vyao bila kupenda bali kwa unafiki kwa vile wanajua wanalambalamba chochote kutokana na vyama hivyo. Shime sasa tuukatae umasikini huu tulio nao wa viongozi.Sina haja ya kurudia maneno ambayo wananchi wengi wanayaongea viongozi kujilimbikizia mali na ubinfsi uliokithiri na kutowajali wananchi ambao wanazidi kumasikinika kila kukicha. Sasa viongozi wa aina hii ni wa kazi gani katika nchi? Wanaona starehe gani kwa kuongoza masikini. Sipendi hata kuongelea juu ya utajiri uliopo katika nchi hii ambao wote uko mikononi mwa viongozi  bila kujali kugawia wananchi wanachostahiki. Najua iko siku kila aliechukua mali ya wananchi atairudisha kwa wananchi apende asipende Mungu hapendi dhuluma. Amini nawaambia siku inakuja haki itatendeka kabla ya kuisha kwa ulimwengu huu.Wananchi tukiamua tunaweza. Wakati sasa umefika wa kuamua tena tumechelewa sana sio kupiga kelele kila siku. Watu husema kelele za chura hazimzuii ng'ombe kunywa maji. Tukijatahamaki maji yote yatakuwa yamekwisha kisimani. Mwenye masikio asikie, na mwenye macho aone

Ni mimi mpenda haki

Tanga.Tanzania

Views: 4

Reply to This


ADVERTISEMENT


TANGAZA HAPA

ADVERTISEMENTS

Latest Activity

Sili Silali liked GLOBAL's blog post PSI YATOA SEMINA YA KUJIKINGA NA MAAMBUKIZI YA UKIMWI KATIKA MABAA NA VILABU YA POMBE JIJINI MBEYA
2 hours ago
Theddy Jacob liked GLOBAL's blog post SETH AFUNGUKIA PENZI LA LULU, KANUMBA
4 hours ago
Saleh Jadid Saleh commented on IL-YA's blog post Dubai:House girl,achanganya mkojo wake na chakula cha mwajiri wake!.Huko Singapore nako wembe ni ule ule!
"Kumbe ww Ilya Upo Iran? nilikuwa sijui mpaka nimesoma profile yako, nakuhurumia kwa kusema uongo…"
8 hours ago
asha liked GLOBAL's blog post Mapenzi ni fursa, iheshimu kwa maana haiji mara mbili
8 hours ago
IL-YA replied to Hussein Marandu's discussion UMMA WA KIISLAM NA KUJENGA JUU YA MAKABURI:Kwanini ukweli huu unafichwa? in the group UKUMBI WA KISLAMU
"Dada Saumu,@ kuhusu kupotea kaburi la mama yako,nakupa pole sana kwa hilo,na hilo limetokana na…"
9 hours ago
chiya left a comment for Jazihina Jaziu
"hi jazihina vipi hali sorry nimechelewa kukujibu  "
10 hours ago
chiya left a comment for chiya
"hi vipi hali sorry nimechelewa kukujibu "
10 hours ago
kajerekani commented on Sili Silali's photo
Thumbnail

Gold digger

"hii ni kali ya mwaka"
11 hours ago
Matata Mpili shared GLOBAL's blog post on Facebook
12 hours ago
Matata Mpili shared GLOBAL's blog post on Facebook
12 hours ago
Matata Mpili shared GLOBAL's blog post on Facebook
12 hours ago
arthur moore commented on IL-YA's blog post Dubai:House girl,achanganya mkojo wake na chakula cha mwajiri wake!.Huko Singapore nako wembe ni ule ule!
"Ooh!! asante IL-YA kwa hiyo habari kweli waarabu sio watu wengi wao hawana utu kabisaa na watoto…"
12 hours ago

© 2012  

Designed & Developed by
G5 CLICK COMPANY.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service

How to make a Website