Yesu wetu apewe sifa ndugu zangu, jamani kunamatamasha ya ujasiliamali ambayo yanajulikana kama Street university ambayo huedeshwa na akina Erick Shigongo, matamasha haya yameleta sura mpya baada ya waimbaji wa Neno la Mungu kama: Christina Shusho, Bonny Mwaitege, Abass Hamis Kinzasa, Glorious Singers na Pastor Wambura. kuonekana wakitumbuiza katika moja ya matamasha hayo lililofanyika mjini Arusha 27 November 2011. watu walifurika na walifurahi kwa kile walichokiita ni Burudani kutoka kwa waimbaji hao, jamani waimbaji hii si halali, ninyi mmeitwa na Mungu ili mmwimbie Mungu, yeye Mungu hajawaita muwaimbie wajasiliamali wala kuimba kwa kuwaburudisha wanadamu! hii sio sahihi kabisa, tena mnakutanishwa jukwaa moja na waimbaji wa Duniani wenye kusifu zinaa! si vizuri nyinyi muimbe pamoja na waimbaji wa ki-dunia katika jukwaa moja mkisisitiza jambo flani kwa nia moja huku wenzenu wakiimba nyimbo za kusisitiza uasherati, au ndio mtaniambia "Mwanasimba atalisha pamoja na mwanakoo siku za mwisho?" Jamani hawa wajasiliamali dhamira yao sio kumtukuza Mungu ila ni kujipatia wateja katika programu zao, sasa wanawatumia nyinyi kama vivutio vya wateja wao.
Ndugu zangu katika Bwana, hebu tafakarini katika hili, mumejikwaa acheni kufanya hivyo.
Na Nyinyi Wajasiliamali acheni kuwatumia waimbaji wa Mungu katika kampeni zenu. Tena kama wewe Erick unamjua kabisa Mungu vizuri lakini Shetani unampa Nafasi akuvute ili uzidi sana katika kumchukiza mungu! acha mara moja. Tafuta njia mbadala ya kuvuta wateja lakini usitumie chochote kitokacho Madhabahuni kwa Bwana, kama unasikio na usikie Acha kabisa usirudie tena.
Bwana awasaidie katika jina la Yesu.
=======================================================================
Ndugu msomaji tunaomba mtazamo wako na uelewa wako kuhusu jambo hili, je wewe unasemaje katika hili, Ni sahihi? Tuandikie maoni yako katika katika E-mail ifuatayo:
mosesmayila@yahoo.com
Au toa maoni yako moja kwa moja kwenye mtandao: www.mosespk.wordpress.com
Tags:
| 1 |
GLOBAL |
| 2 |
julius manning |
| 3 |
Man KKK |
| 4 |
chama baby |
| 5 |
Sili Silali |
| 6 |
IL-YA |
| 7 |
msichoke mlugu |
| 8 |
mohd nasser |
| 9 |
Maji Marefu |
| 10 |
Hellen Attarsingh Gupta |
Sili Silali liked GLOBAL's blog post PSI YATOA SEMINA YA KUJIKINGA NA MAAMBUKIZI YA UKIMWI KATIKA MABAA NA VILABU YA POMBE JIJINI MBEYA
Saleh Jadid Saleh commented on IL-YA's blog post Dubai:House girl,achanganya mkojo wake na chakula cha mwajiri wake!.Huko Singapore nako wembe ni ule ule!
IL-YA replied to Hussein Marandu's discussion UMMA WA KIISLAM NA KUJENGA JUU YA MAKABURI:Kwanini ukweli huu unafichwa? in the group UKUMBI WA KISLAMU
chiya left a comment for Jazihina Jaziu
arthur moore commented on IL-YA's blog post Dubai:House girl,achanganya mkojo wake na chakula cha mwajiri wake!.Huko Singapore nako wembe ni ule ule!
