Ni matumaini yangu kuw hamjambo, poleni na majukumu mengi ya ujenzi wa Taifa letu.
Ikiwa ni mara yangu ya tatu tu kuweka mjadala humu, leo nimekuja na jambo ambalo binafsi kama mtumishi wa serikali limenigusa sana tu. ni kuhusu kodi kubwa tunazotozwa watumishi. nitachukulia mfano wa mtumishi anayelipwa laki sita kwa mwezi kodi anayotozwa inafikia kiasi cha chilingi 97,000/= kila mwezi.kwa mwaka mmoja ni 1,164,000/=
binafsi nilikaa na kuchambua kodi zingine za nyongeza anazokatwa huyu mtu nikaona ya kuwa tunibiwa bila ya kujua tukiwa tunachekela mwizi wetu.
Hebu kwa haraka tu niwajuze hili.
Umeshalipa laki moja kama kodi ya PAYE bado ukienda dukani kuna 20% VAT
 kwa kila unachonunua.
Ukipanga nyumba napo kuna kodi ya pango ambayo imeingizwa hivi kaibuni, ukiendesha gari lako kuna kodi kubwa tu unatakuwa kulipia pale TRA, ukisafiri vilevile,
ukiangalia mbunge anayelipwa milioni 12 kwamwezi hakatwi kodi hata senti, bado huyu ana marupurupu mengi tu. akimaliza muda wake anapewa milioni 40, kwa muda wa miaka5 tu. na kipindi kijacho itakuwa hivyo.na wengine ndo kama tunavyowaona kwena kupiga meza na kulala mjengoni.
Serikali yetu inge angalia utaratibu wa kila mfanyakazi akawa na TIN namba yake anapofika dukani anaonyesha na bei anayouziwa inakuwa bila VAT . ama ungeandaliwa utaratibu wa kompyuta zikafanya kazi kama hii,.

Views: 6

Reply to This

Replies to This Discussion

helow bro,unayosema ni kweli kabisa,na ukizingatia hasa katika sekta watu binafsi wanaokuja kuekeza.JAMANI YAANI UONEVU MTUPU WAKUBWA ZETU WANAO TUFANYI(WALOSHIKA MADARAKA KTK NCHI)yaani mtu anatoka nchini kwake na kuja kuchuma kwetu na pia kuchukuwa nguvu za mwananchi na pia kwa mshahara mdogo na hapohapo serekali pia anachukua kodi.hawatizami nguvu za mtanzania na mali zetu.jee ni haki?eti tuna vyama vya kututetea kama tuico na kadhali ila watu hawa mbona hawafatilii?mishahara mibovu,matusi ya kunyanyaswa na kazi nyingi mbali ya makubaliano na hata over time au lunch hupewi na tunafanya kwakuangalia hatuna pa kwenda na tuna familiya inatusubiri,jee jamani tunasema nchi yetu ina amani,ni kweli ina amani au tuna uwawa huku tunajiona?watu wanagombea viti eti kura(mi simpi mtu kula maana sio kura ni kula)inanitia hasira sana nikizingatia nilivyokuwa uwarabuni natuwa kama mtumishi na mwenye nchi akikuona umeekaa hospitali na hakuna siti ndugu yangu utaamka umpishe yeye akae si kwake?ila sisi mkaribishe mgeni ili atutawale na anakuwa na power kuliko wewe mwananchi.jee ni haki/ama kweli viongozi wanasahau majukumu yao na hawakumbuki kama madaraka ya ukubwa ni dhamana kwa mungu
tatizo watanzania tunajua haki zetu lakini hatuna wa kutupa haki kwani kiukweli kuna vitu pia hatufanyi uchunguzi wa kina si kila mtu anaponunua kitu ahjui kuwa kuna bei ya vat ila kwa kuwa kitu hicho kila mtu anahitaji hana jinsi ya kukataa na viongozi nao hawalioni hili swala kwani wanachoangalia ni maslahi yao Waswahili husema mvuta kamba huvutia upande wake.tunahitaji kufanya maamuzi yaliyo sahihi katika uchaguzi na wale wanaozembea tuwe tayari kuwabainisha.na kinachotugharimu zaidi ni woga wa kumwambia mtu ukweli tunakuwa tayari kumwamini kiongozi kwa haraka bila kufikiri kwa kina
Ni kweli kabisa lzm serikali iangalie hili suala la kodi linaumiza sana.
Kweli kabisa unajua tunalipa kodi mara mbili wafanyakazi?!
Serikali inahitaji kuchakachua system zake kwa ajili ya kuwasaidia wananchi, la sivyo kuna siku tutalipia hadi pumzi tuvutayo.

Mwenzetu umenena! ukiacha PAYEE bado kuna ada za vyama vya wafanyakazi, jamani hivi navyo vinakata pesa yetu nyingi sana, hili nalo litazamwe kwa kina. Nimeona wenzetu wa Ghana, mfanyakazi anaponunua kitu / bidhaa dukani anaonesha ID yake anauziwa hitaji lake bila kodi, hii ni kwa sababu anahesabiwa kuwa alishalipa kodi. Hapa kwetu kodi tunayokatwa haileti mantiki maana kila kitu tunalipia kodi, labda ubahatishe kununua gari mara moja kwa miaka minne ndo utapata msamaha.

UKIYAWAZA SANA HAYA UNAWEZA KUJIKUTA UNALIA MWENYEWE CHUMBANI. MAUMIVU YA MFANYAKAZI NI MAKALI. KODI YA MFANYABIASHARA AKIFIKISHA MILLIONI 10 KWA MWAKA UJUE HIYO NI BONGE LA BIASHARA INAYOINGIZA MAMILLIONI KWA MWEZI, KUMBE KWA MFANYAKAZI, NI MSHAHARA ULIO CHINI YA MILLIONI MOJA. CHA AJABU SASA, PALE UNAPOFANYA KAZI KWA MWEKEZAJI ALIYESAMEHEWA KODI, WEWE NA TUSENTI TWAKO BADO WANAKUFULIGISA NA BONGE LA KODI, SASA HII NI NINI? KICHEKESHO ZAIDI NI KUWA MSAMAHA WA KODI NI KWA MWEKEZAJI MKUBWA WA NJE TU, WA NDANI HATA AWE NA MTAJI KIASI GANI NI KUKANDAMIZA TU!! JAMANI, HIVI KUUFURAHIA UHURU WAKO MPAKA WOTE TUWE BUNGENI?  KWELI NDIYO MAANA KILA MTU ANAOTA KUWA MBUNGE AISEE!

Mi nafikiri serikali haijaamua kulifanyia kazi hili. Lakini serikali inayojali watu wake inapaswa kutokaa kimya. Wakati umefika wa serikali yetu kuliangalia suala hili kwa upya kwani baadhi ya wafanyakazi wanalipa kodi kubwa hata kuliko wafanyabiashara ambao kipato cha mwezi ni zaidi ya mshahara wake mara tano. kwenye kodi haswa PAYE wafanyakazi wengi ni kweli wanadhulumiwa kabisa na hivyo kushindwa kujiletea mandeleo na kufikia malengo waliokusudia.

KODI TUNAYOWEKEWA NA SERIKALI NI KUBWA MNO,HUU NI UONEVU NA WIZI

matatizo hii its happen to alot people even kaka yangu anafanya kazi monday to sunday kwamshara mdogo . kuna wengi wanahangaika just to supporting there family.. its hard and goverment wanatakiwa wabadilishe ..

KWELI KABISA  WAFANYAKAZI TUNAIBIWA

RSS


ADVERTISEMENT


TANGAZA HAPA

ADVERTISEMENTS

Latest Activity

Sili Silali liked GLOBAL's blog post PSI YATOA SEMINA YA KUJIKINGA NA MAAMBUKIZI YA UKIMWI KATIKA MABAA NA VILABU YA POMBE JIJINI MBEYA
2 hours ago
Theddy Jacob liked GLOBAL's blog post SETH AFUNGUKIA PENZI LA LULU, KANUMBA
4 hours ago
Saleh Jadid Saleh commented on IL-YA's blog post Dubai:House girl,achanganya mkojo wake na chakula cha mwajiri wake!.Huko Singapore nako wembe ni ule ule!
"Kumbe ww Ilya Upo Iran? nilikuwa sijui mpaka nimesoma profile yako, nakuhurumia kwa kusema uongo…"
8 hours ago
asha liked GLOBAL's blog post Mapenzi ni fursa, iheshimu kwa maana haiji mara mbili
8 hours ago
IL-YA replied to Hussein Marandu's discussion UMMA WA KIISLAM NA KUJENGA JUU YA MAKABURI:Kwanini ukweli huu unafichwa? in the group UKUMBI WA KISLAMU
"Dada Saumu,@ kuhusu kupotea kaburi la mama yako,nakupa pole sana kwa hilo,na hilo limetokana na…"
9 hours ago
chiya left a comment for Jazihina Jaziu
"hi jazihina vipi hali sorry nimechelewa kukujibu  "
10 hours ago
chiya left a comment for chiya
"hi vipi hali sorry nimechelewa kukujibu "
10 hours ago
kajerekani commented on Sili Silali's photo
Thumbnail

Gold digger

"hii ni kali ya mwaka"
11 hours ago
Matata Mpili shared GLOBAL's blog post on Facebook
12 hours ago
Matata Mpili shared GLOBAL's blog post on Facebook
12 hours ago
Matata Mpili shared GLOBAL's blog post on Facebook
12 hours ago
arthur moore commented on IL-YA's blog post Dubai:House girl,achanganya mkojo wake na chakula cha mwajiri wake!.Huko Singapore nako wembe ni ule ule!
"Ooh!! asante IL-YA kwa hiyo habari kweli waarabu sio watu wengi wao hawana utu kabisaa na watoto…"
12 hours ago

© 2012  

Designed & Developed by
G5 CLICK COMPANY.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service

How to make a Website