Tanzania hakuna wanasiasa,wote njaa tu na ulevi wa sifa ndo vinawasumbua! mwanasiasa ni mtu wa kuona mbali,sasa wenzangu na mimi wanataka kuingia madarakani au wapo madarakani kwa visera vyao vya miaka mitano mitano,tutafika wapi. Vi-sera vyao ukivisoma kwanza sio representative kwa mawazo na mahitaji ya watanzania wote, pili viko kama bajeti za kuendeshea kay moja tu na sio taifa!

Na ndo maana wanatuingiza katika mikataba ya kihuni isiyokuwa na tija kwa taifa,sababu hawaoni mbali,pia uwezo wao wa kufikiri na kuongoza ni wa kiwango cha familia tu na sio taifa!

Linapotokea tatizo hukurupuka na kutafuta shortcut kuficha tatizo,matokeo yake ndio hayo ya kuilipa DOWANS pesa ambazo tunazihitaji sana katika kipindi hiki,au yale ya kuanzisha bodi ya mikopo bila kujua itafanya kazi gani,wala kujua ugumu wa kazi ulivyo,wanakaa na kula pesa tu katika vikao,wakiwaacha vijana wanahangaika na masomo bila hizo pesa walizo sema watawapa. Hii ni aibu sana kwa taifa lenye miongo kadhaa tangu uhuru!

Umasikini tunaotakiwa kupigana nao kwa sasa,sio wa mali/pesa bali ni wa kukosa viongozi wenye maono (Vision) ambao ndio kimekuwa kikwazo kikubwa cha maendeleo ya taifa hili.

Adui mkubwa wa watanzania sasa sio Maradhi,umasikini na ujinga,kama alivyosema Mwl JK Nyerere, bali ni hao wapiga porojo wanaojiita viongozi/wanasiasa na hali uongozi hawaujui na hata hawajui siasa.

Tanzania sio masikini,kinachokosekana ni vipaumbele,hakuna hata siku moja,tukaweza kufanya vitu vyote kwa wakati mmoja,matokeo yake yatakuwa duni kwa sababu kutakuwa na divided attentions ambazo zitapelekea kupungua kwa ufanisi kwa kila kitu tunachogusa kufanya kama taifa,ambayo ni upotezaji wa rasili mali kama tunavyoona sasa!

Ukweli ni kwamba rasili mali kubwa kwa nchi yoyote ni watu,ndo maana nchi kama Canada na zingine za ulaya wanashawishi watu wahamie huko wapewe uraia ili watumike katika kujenga uchumi, je katika hili tanzania tutasema ni masikini na hali tuko 40milion. Rasili mali nyingine ni ardhi, je katika hili tutajitetea vipi? Kama kweli sio fikra mgando za hao wanaojiita viongozi wetu!

Aaaaaaaaagh! inaudhi bwana,hebu tufikirie kidogo nje ya box ili twende mbele. Sio lazima kuiga kila kitu kutoka nje ili kuendelea, wako wasomi watu hebu tuwatumie.

Viongozi wa tanzania wasikilizeni wananchi,na hasa hao wasomi na wenye uelewa,wanayo majibu sahihi ya matatizo yao/yetu. Na sio nyie kila kukicha mnajifungia kwenye vikao mkidhani mnaweza kuleta maendeleo ya tanzania kwa vikao na posho mnazojilipa! Na wala sio safari zenu za nje za kila siku ambazo kiukweli hazina faida kwa mtanzania wa kawaida.

Enyi viongozi,vueni hiyo miwani mlo vaa,manake mnakotupeleka kuna bonde kubwa,tutatumbukia humo na hatutapata wa kututoa,acheni kujifanya viziwi.

Ndimi Mkaapembeni!

Views: 1546

Reply to This

Replies to This Discussion

WAPIGAPOROJO

Tumeyataka wenyewe, mataifa yalitushangaa kumpoteza mtu kama SALIM AHMED SALIM, viongozi wazalendo wapo ila wanadhibitiwa.

hizi ni porojo tuuu(siasa haina mpango,hasa pale viongozi wanapokuwa waongo,hasa viongozi wetu)

RSS

ADVERTISEMENT


Advertisement

 

Forum

KIPIGO CHA BAO 2-1 KWA MAN UTD, KOSA LA MWAMUZI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Mohammed Mar 26. 6 Replies

JE, NI KWELI KWAMBA KIPIGO CHA BAO 2-1 ILICHOKIPATA MAN UTD KUTOKA KWA REAL MADRID USIKU WA KUAMKIA LEO LAWAMA ZOTE ZIMWENDEE MWAMUZI WA MCHEZO AU MAN UTD WAJILAUMU WENYEWE? TUPE MAONI YAKO!!!

HALI INAYOENDELEA BUNGENI, SPIKA NA NAIBU WAKE WAMESHINDWA KUONGOZA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Ali Abdalla Ali Apr 22. 20 Replies

Tumeshuhudia kwa siku za hivi karibuni hali halisi iliyokuwa inatokea katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, kwa hali hii ni ishara kuwa Spika na Naibu wake washindwa kuliongoza bunge hilo?

VURUGU ZA CCM NA CHADEMA KUGOMBEA MLINGOTI WA BENDERA DODOMA, NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Phinehas Rishiansia Kileo May 3. 6 Replies

Wafuasi wa CCM wakimshambulia mfuasi wa Chadema mkoani Dodoma…

Tags: BENDERA, WA, DODOMA, NANI, KULAUMIWA?

VURUGU ZINAZOENDELEA HAPA NCHINI NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by NELSON UVAMBE on Monday. 27 Replies

HIVI KARIBUNI KUMEKUWEPO UPOTEVU WA AMANI HAPA NCHINI PAMOJA NA WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI. MKOANI KAGERA WANANCHI WENYE HASIRA WALIWAUA POLISI, IJUMAA ILIYOPITA WAKULIMA NA WAFUGAJI HUKO WILAYANI KILOSA WALIZUA VURUGU NA KUFUNGA BARABARA,…

MRISHO NGASSA KUPELEKWA SIMBA SC BILA RIDHAA YAKE, JE NI HALALI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Domino Bagambisa Jan 21. 17 Replies

Kiungo hatari wa Azam FC, Mrisho Ngassa leo amepelekwa Simba SC kwa mkopo na timu yake…

Tags: SOKA

hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Started by Gysper in Siasa. Last reply by Jamal amor May 9. 24 Replies

 hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Kauli Ya JK kuwa Mauaji ya Arusha ni "Bahati Mbaya"

Started by Kulikoni Ughaibuni in Siasa. Last reply by richardngeze Feb 12. 12 Replies

Tanzania tuna tatizo kubwa.Hakuna haja ya kunyoosheana vidole as to nani amechangia tatizo hilo bali cha muhimu na haraka ni namna tutakavyoweza kutatua tatizo hili.Nisimung'unye maneno: tatizo kubwa linaloikabili ni kuwa na Rais ambaye takriban…

© 2013   Created by Global Publishers.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service