HIVI KWELI VIONGOZI WETU WANA UCHUNGU NA WANANCHI WANAOSAFIRI KUPITIA RELI YA KATI?

Leo asubuhi kwenye taarifa ya habari kupitia television ya Taifa niliona kitu cha ajabu,pale nilipoona mpaka watoto wanahojiwa taabu wanayopata kupitia kukwama kwa safari yao kwa njia ya treni kwa mvua zinazoenelea kunyesha sasa,daraja la treni limeanza kuzama na hivyo kupelekea safari za treni kupitia njia hiyo kusimamishwa!!! kinachoniuma hapa ni ile hali ya wananchi kuendelea kuibiwa na kulala njaa huku wakingoja serikali iwaletee mabasi ya kuwanasua au kuwasafirisha kutoka hapo walipokwama.Jamani ungeona mambo yalivyokuwa mngeguswa sana...nashauri serikali kuwa makini au kufanyia uchunguzi barabara na reli hasa kipindi hiki cha mvua.NI HAYO TUU KWA LEO

Views: 2198

Reply to This

Replies to This Discussion

Tatizo ni lile lile, fikra mgando kwamba kila kitu lazima aje mwekezaji ndo mambo yaende,ona sasa yanayotokea. Mwekezaji kapewa hajali hata kufanya survey kuweza ku-anticipate ni wapi panaweza kutokea tatizo katika mfumo mzima wa reli.

Mwekezaji mara zote ana lengo moja tu akilini,kutengeneza faida na sio kujali na kuhakikisha miundo mbinu iko sawa.

Hivi shida yetu siku hizi nini jamani! mbona mkoloni aliwatumia babu zetu kiujenga hiyo reli ambayo tunatumia hadi sasa,sisi tunashindwa nini kama sio kithibitisho kuwa kuna matatizo ya kimaono kwa viongozi wetu.

Leo ni mvua, kesho itakuwa ni moto na wala hakuna hata hatua zinachukuliwa kumhakikishia msafiri wa hiyo reli kuwa likitokea la kutokea kua maandalizi ya kutatua tatizo haraka!

Kama mkoloni aliweza sisi tunashindwa nini kujenga nyumba yetu wenyewe katika kipindi hiki tunasema tuko huru na tekinolojia inatusaidia?

Mimi naona kuna shida hapo ya umbali kati ya wanaojiita viongozi na wanachi kufikia kiasi cha wao kushindwa kuwashawishi watu kufanya jambo kwa manufaa ya taifa zima. Na ukiona hivyo ujue tunakoelekea sio kwema sana.

Mungu ibariki Tanzania.

hahahaha du kaka umesahau ule usemi usemao kila mtu anakula kutokana na ulefu wa kamba yake. sahau hayo hakuna atakae jali.

WAKINA JAKAYA KIKWETE WANATAKA KURA TU HAKUNA KINACHOFANYIKA

 

Mwisho wa matatizo ya reli ni 80% kuibinafsha, kuwapa watu bunafsi walimbike kwenye shirika hilo. Kwea njia hii ulaji na uzorotaji utakomeshwa.... Kwa sababu iwapo watu binafsi watakuwa na hisa katika shirika hili watakuwa makini kuangalia kwamba hawaibiwi ndo maana wenzetu vitu vyao vina endlea. Chukuwa mfano Kenya Airways ina ubia na KLM ya Uholanzi.

Ndege ilikuwa inayomilikiwa na Serikali ya Kenya hadi Aprili 1995, na ili binafsishwa mwaka 1996, kuwa Shirika hilo kwa sasa ni la ushirikiano wa serikali na sekta binafsi. Mbia mkubwa ni KLM (26%), ikifuatiwa na Serikali ya Kenya, ambayo ina hisa 23% na wamiliki binafsikama  Nairobi Stock Exchange, Dar-es-Salaam Stock Exchange, na Uganda Securities Exchange.Kwa hali hii KLM hatokubali watu wale tu. wabia binafi watakuwa macho. Lakini Reli ya kati pamoja ma makampuni mengine yana milikiwa na serikali.... Hivi ni KULA KULA KULA KULA LAKINI usionwe na wengi wanaoshika ngazi za juu wanacheza kiwanja kimoja.

Na kama tutataka kubinafsisha basi ubinafsishaji uwe na watu wanao eleweka mfano mwaka  2007 mkataba  RITES Ltd. ya india kuendesha reli hiyo serikali ikawa na hisa ya 46%. Its just crazy watu wa serikalini. Kuna watu ambao hawana viwango na uwezo wa kundesha kampuni katika nchi yetu. Arrrrgh na pata vidonda vya tumbo!

 

Kwa nini wawe na uchungu wakati wenyewe wanatumia magari ya serekali. Sijui wanaotumia usafiri huo. Zingatia pia kupanda kwa bei ya vitu kwa mikoa ya Singida, shinyanga, Mwanza, Bukoba na kigoma ni kutokana na usafirishaji kuwa aaghari. Kama kweli viongozi wetu wangekuwa na uchungu na raia wenye hali duni wangetengeneza reli kurahisisha usafiri. Sasa kubwa ni kwamba viongozi wana biashara ya malori treni likipona watakosa biashara ndio maana hawapendi kutengeneza reli.

 

Kwa kuwa na mimi ni mhanga wa reli ya kati basi naona kuna umuhimu wa kuchangia mada hii. Ndugu yangu laiti ungeliona jinsi mchakato wa kujenga reli ya kati enzi hizo ungelijua ni jinsi gani watu waliohusika na ujenzi wa taifa wakati huo walivyokuwa commited. Mchakato ulikuwa too machenical ni sululu, jembe na kubeba reli begani. Leo tuna ma bull dozers, earth movers, crane za kubeba reli na utitiri wa vifaa ambavyo technolojia imetujalia  angalia yanayotokea. Sio kujenga reli tunashindwa kukarabatii!!! hebu tujiulize tatizo ni nini? Utaona dhahiri tatizo ni viongozi wanaojali maslahi yao zaidi kuliko maslaya taifa. Kwanza wameuza mashirika yetu bila kutushauri kwa kisingizio kuwa serikali inajitoa katika kufanya biashara. Lakini bei ya kujiuzua ni sawa na bure. Haya baada ya kuuza nini kinafuata ni kila mtu kujichotea. kwa kifupi ni kwamba reli ya kati na hasa ya kwenda kigoma ni bora watanzania mkasahau kwa sababu wakubwa wanasafiri kwa ndege na magari ya kifahari sisi kina kajamba nani tunalazimika kusafiri na treni na treni yenyewe si lolote si chochote unaweza kusafir kwa wiki mbili kutoka Dar kwenda Kigoma. Siku moja nilikuwa nasafiri nikitokea Kigoma kwenda Morogoro kwa mara ya kwanza nilishuhudia Treni ikiishiwa dizeli kama gari kweli nilishangaa sana. Nikasema kweli Tanzania imekwisha na Ukistajabu ya Musa Utaona ya firauni

 

SASA MLITAKA RAIS AFANYE NINI?

hawawajibishe wahucka

hapana mi naona hawana uchungu,na wala hawana mwelekeo wakuwa na uchungu hivyo basi watanzania ni wakati wa kufunguka hawa jamaa waachie dola 2015,ili wachukue wale wenye uchungu na wananchi wao,

Wanasiasa wapo wengi tu ila wanadhibitiwa, mnakumbuka zengwe alilopandikiziwa mzee wetu SALIM AHMED SALIM katika kinyang'anyiro cha nani ateuliwe kupitishwa katika nafasi ya kugombea nafasi ya urais toka ndani ya chama tawala mwaka 2005?

KUSEMA UKWELI INAHUZUNISHA KUONA VIONGOZI WETU HAWANA UCHUNGU NA WANANCHI WANAOSAFIRI KUPITIA RELI YA KATI.NAFIKIRI YOTE HII INATOKANA NA KWAMBA WAO SIO WAHANGA.NAWASHAURI WABADILIKE.

RSS

ADVERTISEMENT


Advertisement

 

Forum

KIPIGO CHA BAO 2-1 KWA MAN UTD, KOSA LA MWAMUZI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Mohammed Mar 26. 6 Replies

JE, NI KWELI KWAMBA KIPIGO CHA BAO 2-1 ILICHOKIPATA MAN UTD KUTOKA KWA REAL MADRID USIKU WA KUAMKIA LEO LAWAMA ZOTE ZIMWENDEE MWAMUZI WA MCHEZO AU MAN UTD WAJILAUMU WENYEWE? TUPE MAONI YAKO!!!

HALI INAYOENDELEA BUNGENI, SPIKA NA NAIBU WAKE WAMESHINDWA KUONGOZA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Ali Abdalla Ali Apr 22. 20 Replies

Tumeshuhudia kwa siku za hivi karibuni hali halisi iliyokuwa inatokea katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Je, kwa hali hii ni ishara kuwa Spika na Naibu wake washindwa kuliongoza bunge hilo?

VURUGU ZA CCM NA CHADEMA KUGOMBEA MLINGOTI WA BENDERA DODOMA, NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by Phinehas Rishiansia Kileo May 3. 6 Replies

Wafuasi wa CCM wakimshambulia mfuasi wa Chadema mkoani Dodoma…

Tags: BENDERA, WA, DODOMA, NANI, KULAUMIWA?

VURUGU ZINAZOENDELEA HAPA NCHINI NANI WA KULAUMIWA?

Started by GLOBAL in Siasa. Last reply by NELSON UVAMBE on Monday. 27 Replies

HIVI KARIBUNI KUMEKUWEPO UPOTEVU WA AMANI HAPA NCHINI PAMOJA NA WANANCHI KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI. MKOANI KAGERA WANANCHI WENYE HASIRA WALIWAUA POLISI, IJUMAA ILIYOPITA WAKULIMA NA WAFUGAJI HUKO WILAYANI KILOSA WALIZUA VURUGU NA KUFUNGA BARABARA,…

MRISHO NGASSA KUPELEKWA SIMBA SC BILA RIDHAA YAKE, JE NI HALALI?

Started by GLOBAL in Burudani. Last reply by Domino Bagambisa Jan 21. 17 Replies

Kiungo hatari wa Azam FC, Mrisho Ngassa leo amepelekwa Simba SC kwa mkopo na timu yake…

Tags: SOKA

hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Started by Gysper in Siasa. Last reply by Jamal amor May 9. 24 Replies

 hivi ni nani yuko sahihi kuhusu uchaguzi wa UMEYA arusha CCM au CHADEMA?

Kauli Ya JK kuwa Mauaji ya Arusha ni "Bahati Mbaya"

Started by Kulikoni Ughaibuni in Siasa. Last reply by richardngeze Feb 12. 12 Replies

Tanzania tuna tatizo kubwa.Hakuna haja ya kunyoosheana vidole as to nani amechangia tatizo hilo bali cha muhimu na haraka ni namna tutakavyoweza kutatua tatizo hili.Nisimung'unye maneno: tatizo kubwa linaloikabili ni kuwa na Rais ambaye takriban…

Latest Activity

tina babi left a comment for kihongosi joel
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
10 seconds ago
tina babi left a comment for Josephat william
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
20 seconds ago
Jeremy Wilke posted a status
""
31 seconds ago
Jeremy Wilke posted a status
31 seconds ago
tina babi left a comment for Mzee kimolodeaf
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
35 seconds ago
Jeremy Wilke posted a status
"Tupe mpya yako ya leo....."
38 seconds ago
tina babi left a comment for Innocent Kalolo
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
1 minute ago
tina babi left a comment for thomas kabutta
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
1 minute ago
Jeremy Wilke posted a status
"Tupe mpya yako ya leo....."
1 minute ago
Jeremy Wilke posted a status
1 minute ago
tina babi left a comment for kevin robert
"tinalutunku@yahoo.com Hello, My name is Miss tina lutunku. i saw your profile today and become…"
1 minute ago
Jeremy Wilke posted a status
1 minute ago

© 2013   Created by Global Publishers.

Badges  |  Report an Issue  |  Terms of Service